Saturday 25 May 2013

MWALIMU MJASILIA MALI......

Mwalimu aliyejitoa muhanga kuishi porini

Mwalimu Salvius Nindi (40)  wa shule ya msingi  Mkenda iliopo mpakani wa Tanzania na Msumbiji akiwa katika moja  ya nyumba zake za kitalii anazojenga kwaajili ya kuboresha kipato chake.
mwalimu huyo haonyeshi masikitiko wala kusita pale alipopangiwa kufundisha katika mazingira ya porini kama ambavyo walimu wengine hukumbia na kuacha kazi wakipangiwa katia maeneo yenye mazingira magumu. yeye anadai kuwa ukiyazoea mazingira magumu na kuyakubali yatakubadirisha maisha yako kama ambavyo yeye alitumia mapori kwa kilimo na sasa ni mfanyabishara mkubwa na anaipend akazi yake.
yeye anawashauri walimu wenzake kutokwepa mazingira magumu kwani kazi ni popote kinachotakiwa tu kuwa wabunifu kulingana na mazingira na kujishughulisha na kazi za ziada badala ya kutegemea kipato cha kazi pekee.
Hata hivyo mwalimu huyu anaishauri serikali kuwafikiria zaidi kwa posho walimu wanaofanya kazi katika mazingira magumu ili kuwatia moyo.

1 comment:

  1. Tunampongeza mwalimu kwa juhudi zao za kupambana na makali ya maisha kwani maisha ni popote kwani bora kazi yako iende vizuri.....

    ReplyDelete