Tuesday 17 December 2013

Mangariba 38 wakamatwa Moshi Tanzania.......







SIMBA WA TANZANIA
UKEKETAJI MARUFIKU ..TZ
Mangariba 38 wakamatwa Moshi Tanzania.......

Maafisa wakuu mjini Moshi Tanzania, wamewakamata wanawake 38 waliopatikana wakiwakeketa wasichana katika eneo hilo......

Kwa nini ukeketaji unaendelea katika baadhi ya sehemu Tanzania licha ya kuharamishwa na serikali?

KABILA LA KIHAYA





MIAKA NA MAANA ZAKE KWA
KABILA LA KIHAYA…TUNA ANZIA MWAKA 1959..

SIMBA JIKE NA DUME.
 1959….BILEMAPLENGILE,                                                  
1960….IJA- OYOBONELE,
1961….BILYE- OYOKOMILE,
1962….GUMYA- OMWOYO,
1963….OTURA- OBUNGYA,
1964…KARAMANSHANYO,
1965..NDALWEBOINE,
1966..BABINDANGILE,
1967..TEKANA,
1968….TABARO,
1969….NYINKILA,
1970…..TWEYAMBE,
1971……SISIMUKA,
1972…….SHAYA,
1973………GENDELELA,
1974………WEKEBUKE,
1975………KAKIWEYO,
1976…….IJA-BALEBE,
1977……..HENJUZA,
1978……..SHULIZA,
1979………TIKILIWA-IGAMBA,
1980……….BURULA-OBONE,
1981……….GALAZIWA –ENZII,
1982………..GOSHOKO,
1983………………………SHOBOKERWA
1984………………………...IKINGULA,
1985……………………..KANKWEANUZEO,
1986……………………..SHUUBILA,
1987……………………….WEMOGE,
1988…………………………KAKUNTANTALIKWA,
1989………………………..KWATILA-AHO,
1990………………………..HANULILWA,
1991…………………………HUMULA,
1992………………………..NYINA-ELIHO,
1993………………………..YOMBEKA,
1994………………………..HUMBYA,
1995………………………GUMA,
1996………………………WECHUZE,
1997……………………….CHAAZIKA,
1998………………………..TEKEREZA,
1999………………………..FIKAMA
2000……………….SHANDUKA
2001…………………..SHAMULA,
2002…………………..RUNDANA,
2003…………………..YEBAZE,
2004…………………….SHAABUKA,
2005……………………SIIMA,
2006……………………..GIREMILEMBE,
2007……………,………TEGEKA
2008……………………..LASHANA
2009……………………..JWAHUKA,
2010……………………….CHULELA,
2011………………………TONGANA,
2012……………………..WECHONCHE,
2013………………………WEEBANGE
 
DARAJA LA KYAKA-MKOA WA KAGERA

Monday 23 September 2013

MASHAMBULIZI LA WESTGATE NAIROBI

Kenya
 
 
 
 
 
 
 
MASHAMBULIZI LA WESTGATE NAIROBI :
 Tanzania tunajiufunza nini? 
TUMEJIFUNZA NINI (3 photos)
Askari wakiwasaidia raia kujiokoa kwa kuwataka kutambaa badala ya kutembea wima au kukimbiaAskari mwenye silaha akiwaongoza watu waliofanikiwa kuokolewa kutoka kwenye jengo lililovamiwa na magaidi
Askari kanzu wakipambana ndani ya Westgate Mall katika harakati za kuwaokoa mateka
Matumizi mabaya yz siraha

Monday 16 September 2013

Serikali imeshindwa kudhibiti uhalifu wa tindikali nchini?


Namwaga lazi

Hujuma hii!
Matukio ya kumwagiwa tindikali yameendelea kukithiri huku Serikali ikiendelea kutoa ahadi za kudhibiti bila mafanikio.  Hivi karibuni baada ya raia wawili wa Uingereza kumwagiwa tindikali Zanzibar, Serikali iliweka mikakati mikali ya kudhibiti matumizi ya kemikali hiyo, lakini bado matukio hayo yameendelea kuwepo.
Tukio la kumwagiwa tindikali kwa Padri wa Kanisa Katoliki Parokia ya Cheju, Mkoa wa Kusini Unguja, Joseph Mwang’amba ni mwendelezo wa uhalifu huo ambao Serikali imeshindwa kabisa kuudhibiti.
Akieleza jinsi tukio hilo lilivyotokea, Padri Mwang’amba anasema alikuwa nje ya duka linalotoa huduma za mawasiliano ya mtandao (Sun Shine Internet Caffee) liliopo eneo la Mlandege Wilaya ya Mjini Unguja, ndipo alipotokea kijana mmoja na kumwagia tindikali.
Wakati Padri huyo akieleza hayo, Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, ameijia juu polisi kwa kushindwa kudhibiti matukio ya viongozi wa dini na Serikali visiwani humo, kushambuliwa kwa kumwagiwa tindikali huku akilitaka kuwakamata waliohusika na tukio hilo.
Kiongozi huyo wa dini, aliyejeruhiwa maeneo ya usoni, mikononi na kifuani baada ya kumwagiwa tindikali hiyo alisafirishwa jana na ndege ya kukodi ya Shirika la Coastal kutoka visiwani humo hadi Dar es Salaam na baadaye kupelekwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kwa matibabu zaidi.
Kwa upande wake, Padri wa Parokia ya Mtakatifu Joseph, Zanzibar, Thomas Assenga aliyefuatana na kiongozi huyo mpaka MNH, alisema siku za nyuma Padri Mwang’amba alitolewa vitisho na mtu ambaye hamfahamu wakati akienda kutoa huduma katika kituo cha wazee cha Welezo.
Alisema kabla ya kufika kituoni hapo, kuna eneo ambalo nyakati za asubuhi watu hufanya mazoezi barabarani ambapo kuna mtu mmoja alimtolea maneno ya vitisho.
Tukio hilo linafuatia tukio la Agosti 7, mwaka huu ambapo raia wawili wa Uingereza, Kate Gee (18) na Kirstie Trup (18) walimwagiwa tindikali katika maeneo ya Mji Mkongwe, Zanzibar na vijana wawili waliokuwa wakiendesha pikipiki aina ya Vespa.
Waingereza hao walisafirishwa siku tatu baadaye kurudi kwao Uingereza kwa ajili ya matibabu.
Utetezi wa Serikali
Siku tano baada ya tukio la Waingereza hao kumwagiwa tindikali, Serikali kupitia vyombo vyake vya uchunguzi iliwataka wananchi kuisaidia kuwafichua na kutoa ushahidi wa uhalifu huo kwani ni vigumu kuwabaini wahusika.
Kauli hiyo ilitolewa kwa pamoja jana na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Said Mwema, Mkemia Mkuu wa Serikali, Profesa Samwel Manyele na Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali (DPP) Eliezer Feleshi, katika mkutano wao na waandishi wa habari, uliolenga kueleza mikakati ya kupambana na matumizi yasiyo sahihi ya tindikali nchini.
 Mkemia Mkuu, Polisi hawawezi kubaini matukio haya bila ushirikiano wa wananchi kwani Tanzania ni nchi kubwa na ina watu zaidi ya milioni 45. Watu wanaingiza tindikali lakini wapo ambao wanatumia tindikali hiyo kwa matumizi haramu,” alisema IGP Mwema.
Amesema tindikali inaweza kutolewa kwa ajili ya shughuli za viwandani, maabara na usafirishaji na kwamba watu wanapotaka kuitumia kwa ajili ya kufanya uovu wanaweza kugundulika kupitia kwa taarifa zitakazotolewa na wananchi, kwa sababu wanakuwa wamezungukwa na jamii ya watu mbalimbali.
Matukio mengine
Tukio lingine lililoshtua ni lile la bilionea Said Mohamed Saad ambaye ni mmiliki wa maduka ya Home Shopping Centre, kumwagiwa tindikali mwanzoni mwa mwezi Agosti.
Said anaendelea na matibabu nchini Afrika Kusini na inaelezwa kuathirika vibaya usoni, mikononi na kifuani.
Alimwagiwa tindikali Julai 19, mwaka huu akiwa kwenye moja ya maduka yake katika Jengo la Msasani Mall, Dar es Salaam.
Taarifa za siku ya tukio zilibainisha kuwa Said alikuwa akizungumza na mfanyakazi wake muda wa saa moja jioni ndipo akatokea kijana mrefu, mwembamba ambaye alimmwagia kimiminika kinachosadikiwa kuwa ni tindikali.
Ilibainishwa kwamba mfanyakazi huyo wa Said, Hassan Ahmad naye alijeruhiwa kidogo katika purukushani hiyo lakini alipopelekwa Hospitali ya Ami Wellness Centre, alitibiwa na kuruhusiwa huku bosi wake akipelekwa Afrika Kusini usiku huohuo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camilius Wambura anasema matukio ya kutumia pikipiki yanaonyesha kupangwa hivyo inakuwa vigumu kuwabaini wahalifu mapema. 
Tukio hilo linafanana na lile lililotokea Septemba 8, mwaka huu ambapo mfanyabiashara wa vifaa vya ujenzi, Christian Msema wa Mburahati jijini Dar es Salaam, alimwagiwa kemikali hiyo na watu waliokuwa kwenye pikipiki ya matairi matatu.
Msema maarufu kama Mnyalu amelihusisha tukio hilo lilitokea jioni ya Jumamosi Septemba 8 na mgogoro wa eneo la wazi ambapo yeye alikuwa akipinga mfanyabiashara mmoja (jina linahifadhiwa) kulitumia kuegesha magari yake.
Akizungumza kwa shida katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili alikolazwa anakiri kuwa mstari wa mbele kupinga eneo hilo kutumiwa kinyume na sheria.

“Awali vijana wasio na ajira waliomba eneo hilo ili walitumie kwa mradi wa kuegesha magari, wakaandika barua, lakini Serikali ya mtaa ikakataa ikisema hilo ni eneo la kazi. Hiyo ilikuwa mwezi Oktoba mwaka jana, ilipofika Novemva, tukaona malori yanaegeshwa pale. Tulipofuatilia tukaambiwa ni mwenyekiti wa mtaa ameruhusu,” anasema na kuongeza:
“Tukajiorodhesha wana mtaa tukafika kama watu 60 na mimi nikawa mwenyekiti wao, tukapeleka barua yetu kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni ambaye aliipeleka kwa ofisa wa mipango miji.”
Ameongeza kuwa ofisi ya mipango miji ya Kinondoni ilisema hilo ni eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa shule ya sekondari hivyo ikaagizwa kuwa magari hayo yaondolewe. 
“Kampuni iliyopewa tenda ya kuondoa yale magari ilifanya kazi bila kutoa notisi, ndipo yule mwenye magari akaenda kulalamika kwa mkuu wa mkoa. Malalamiko yakafika kwa Mkurugenzi ambaye aliagiza kampuni hiyo irejeshe hayo magari ili utaratibu ufuatwe,” alisema.  Aliendelea kusema kuwa yule mfanyabiashara aliendelea kukaidi kwa kuongeza magari mengine kwenye uwanja huo hadi yalipokuja kuondolewa kwa nguvu.
Msema alisema wakati mvutano huo ukiendelea, aliwahi kukutana na mlinzi wa mfanyabiashara huyo ambaye alimtahadharisha kuwa harakati zake hizo zitamponza kwani anafuatiliwa.
“Mimi sikukata tamaa kwani lile ni eneo la umma kwa nini mtu ang’ang’anie? Lakini watu wengi walinitahadharisha kuwa yule jamaa ananifuatilia, ndiyo maana siku ile ya tukio kuna bajaji kumbe ilikuwa inanifuatilia kwa muda mrefu,” anasema.
Mwenyekiti wa mtaa wa Mburahati, Tungaraza amekanusha kuwepo kwa mgogoro huo huku akimtaka mwandishi afike ofisini kwake kwanza.  Matukio  hayo yameanza muda mrefu na wakati mwingine yamehusishwa na chuki za kisiasa.
Baadhi ya wananchi wanashauri Serikali kuwa imara na tindikali hasa katika chaguzi zijazo, kwani tindikali ni rahisi kuibeba.

twiga

Sunday 15 September 2013

Dawa ya mifugo yatengenezea gongo Dar

Dar es Salaam. Wakati Serikali ikiahidi kuongeza nguvu katika vita dhidi ya wauza dawa za kulevya nchini,
imebainika kuwa kuna mtandao wa wafanyabiashara wa pombe haramu ya gongo unaopika na kuichanganya na dawa za mifugo ili kuiongezea ukali.
Mtandao huo unaomiliki mitambo ya kupika gongo katika eneo la Mto Kizinga uliopo Dambweni, Kata ya Kilungule, wilayani Temeke, unadaiwa kuchanganya pombe hiyo na dawa ya mifugo aina ya Multivitamin ambayo hutumika kurutubisha wanyama.
Hata hivyo, uchunguzi uliofanywa na gazeti hili umebaini kuwa dawa hiyo huchanganywa na dawa nyingine ambayo haikufahamika mara moja, kisha kuiweka kwenye gongo ili kuiongezea ukali zaidi.
Wafanyabiashara hao wamekuwa wakipika gongo hiyo katika eneo hilo kwa miaka zaidi ya 10, huku baadhi ya viongozi wa serikali ya mtaa wakitajwa kuwalinda.
Kwa mujibu wa uchunguzi, eneo hilo lina mitambo zaidi ya minne ya kutengeneza gongo na kila mtambo unazalisha pipa moja lenye ujazo wa lita 200.
Mtambo wa gongo
Uchunguzi ulibaini kuwa kila siku wanazalisha zaidi ya lita 800 za gongo ambayo huuzwa kwa rejareja na jumla. Bei ya rejareja kipimo kinaanzia Sh500 hadi Sh5,000, ambapo bei ya jumla ni Sh38,000 kwa ndoo yenye ujazo wa lita 20.
Kwa mtu anayefika kwa mara ya kwanza eneo hilo atakutana na makundi ya watu wakiwa chini ya miti wakijipumzisha wakati wakisubiri pombe hiyo kuwa tayari, huku wakazi wengine wa eneo hilo wakionekana kuendelea na shughuli zao kwenye bustani za mboga za majani zilizolimwa kando kando ya mto.
Mbali ya kuwa wanalindwa na baadhi ya viongozi wa mtaa, wameweka ulinzi wao wenyewe, kwa kuweka vijana zaidi ya 10 ambao hukaa katika eneo hilo kuhakikisha kuwa mtu anayefika katika eneo hilo wanamtambua.
Ukifika katika eneo ilipo mitambo yao, watu wanaofanya kazi ya kupika ni wacheshi, wanaojaribu kumsalimia kila mpita njia bila ya kuwa na hofu yoyote, huku mmojawao ambaye jina lake halikufahamika mara moja akisema kuwa wao ndio waliotengeneza barabara ya kupita magari inayoingia sehemu hiyo.
Mkazi mmoja wa eneo hilo ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini kwa kuhofia usalama wake, alisema watu hao ndiyo wasambazaji wakubwa wa gongo jijini Dar es Salaam.
“Biashara hii inalipiwa ‘kodi’ kila mwezi, hawa jamaa huchangishana fedha halafu huwapelekea baadhi ya askari ambao huwalinda wasikamatwe, kuna wakati huchanga hadi laki tatu. Vigumu sana kukamatwa,” alisema.
Gongo inavyotengenezwa

Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili ulibaini pombe hiyo inatengenezwa kwa kutumia malighafi mbalimbali ikiwamo mapapai yaliyooza, vitambaa vichafu vilivyovunda, mihogo na wakati mwingine kinyesi cha binadamu hasa wakati bidhaa nyingine zinapoadimika.
Mfanyabiashara mmoja (jina linahifadhiwa) alisema amekuwa akipika gongo na kuigawa katika madaraja matatu; iliyopikwa kwa mapapai yaliyooza ndiyo inayopendwa zaidi na wateja wake ikilinganishwa na iliyotumia malighafi nyingine.
“Sisi tunatumia mapapai yaliyooza, tunaongeza na sukari pamoja na hamira, ikishaiva tunaitenga kutokana na madaraja yake. Gongo ya eneo hili inasifika sana kwa sababu ya ubora wake, hatuna tatizo la ukosefu wa maji kama walilonalo wenzetu ndiyo maana unaona tunaung’ang’ania huu mto hapa,” alisema na kuongeza :
“Kama mapapai yakiadimika sana, tunaweza kupika kwa kutumia vitambaa vichafu au mihogo.”
Akifafanua alisema wamekuwa wakitembea kwenye madampo kuokota vitambaa pamoja na takataka nyingine, kisha huziloweka kwenye maji kwa muda mrefu hadi zivunde ndipo huwa tayari kwa kupikia gongo.
Uchunguzi uliofanywa unaonyesha kuwa mbali ya pombe hiyo kutengenezwa kwa kutumia takataka zinazookotwa kwenye madampo, pia huongezewa ukali kwa kutumia dawa za kuongezea vitamini mifugo.
Mteja mmoja wa pombe hiyo ambaye alijitambulisha kwa jina moja la Sadick, alisema gongo inayopikwa eneo hilo imekuwa maarufu kwa kuwa kuna dawa ya mifugo ya Multivitamin ambayo huongezwa baada ya pombe hiyo kuiva.
“Mimi ninafahamu kuna dawa ya mifugo inawekwa kwenye hii gongo ili kuiongezea nguvu. Sijui ni dawa aina gani, lakini kuna jamaa huwa namwona anakuja kuuza hiyo dawa. Gongo iliyowekwa hiyo dawa inakuwa na nguvu sana,”alisema Sadick.
Mtaalamu wa Mifugo, Joseph Nong’ona alisema wanywaji wa pombe hiyo wapo katika hatari ya kudhurika kiafya kwa kuwa dawa ya Multivitamin inayotolewa kwa wanyama ina nguvu zaidi ikilinganishwa na ya binadamu, na kwamba mtu haruhusiwi kunywa maziwa au nyama ya mnyama aliyepewa dawa hiyo kwa siku tatu.
“Multivitamin anayopewa mnyama ina ‘concentration’ kubwa ikilinganishwa na ile ya binadamu, lakini pia ikumbukwe kuwa ile ni kemikali sijui inakuwaje inapochanganywa na gongo ambayo yenyewe tu ina madhara makubwa kiafya. Kwa kawaida mnyama akipewa dawa hiyo huwa tunashauri asikamuliwe mazima au nyama yake isitumike kwa siku tatu,” alisema Nong’ona.
Akizungumzia biashara hiyo, Katibu wa Mtaa wa Kilungule, Juma Ahmed aliwatetea wafanyabiashara hao kwa madai kuwa hajawahi kupata taarifa zozote za kufanya uhalifu badala yake wamekuwa walinzi wa amani katika mtaa huo.“Ni watu wazuri sana, sijawahi kusikia wamefanya jambo lolote baya, kwanza wamegeuka kuwa walinzi wa amani hapa mtaani kwetu… wanajua biashara wanayoifanya siyo halali kwa hiyo hawataki matatizo na mtu,” alisema Ahmed.
Kamanda wa Polisi wa Temeke, Engelbert Kiondo alisema suala la biashara ya gongo linatakiwa kudhibitiwa na jamii inayowazunguka wafanyabishara hao kwa kutumia ulinzi shirikishi.

“Wanataka kuipa Polisi kazi bure tu, jamii ndiyo inayohusika na suala hilo. Serikali ya mtaa kwa njia ya ulinzi shirikishi wanaweza kuamua kwenda kuvunja mitambo ya gongo,” alisema Kiondo.
Akizungumzia tuhuma kuwa baadhi ya Polisi wanawalinda wafanyabiashara wa gongo, Kiondo alisema tuhuma hizo zimekuwepo muda mrefu na kwamba zimeshapitwa na wakati.

Polisi Simiyu yatoa ripoti ukatili wa Dagashida, fisi wakoleza mauaji



Wiki iliyopita katika ukurasa huu, tuliwaletea mwendelezo wa ripoti maalumu kuhusu mauaji yaliyokuwa yakitekelezwa mkoani Simiyu kupitia Baraza la Kimila maarufu Dagashida na jinsi wananchi wanavyoogopa kutoa ushirikiano kwa polisi.
Leo tunaendelea na sehemu ya tatu na ya mwisho ya ripoti hiyo, pamoja na mambo mengine ikiainisha takwimu za vifo zilizotolewa na Jeshi la Polisi kutokana na matukio mbalimbali ya mauaji ya Dagashida.
Wanakijiji hawatoi ushirikiano
Kamanda Msangi anakiri kuwepo kwa changamoto ya kukosa ushirikiano kutoka kwa wananchi wakihofia usalama wao.
“Sisi tunawaomba wasiogope kutoa taarifa za ukatili huo, lakini pia tunaomba mashirika na dini waendelee kuelimisha,”anasema Kamanda Msangi.
Anaeleza kusikitishwa kwake na viongozi wa kisiasa kutoshiriki katika harakati za kukemea ukatili wa baraza hilo akifafanua tangu alipoanza kazi mkoani Simiyu hajawahi kuona wala kusikia mbunge yeyote wa mkoa huo akikemea ukatili wa Dagashida.
“Hakuna mbunge au diwani yeyote mwenye nguvu ya kuzuia baraza hilo kwa sababu wanalitumia kisiasa, kwa hivyo niwaombe waache kuchanganya siasa na maisha ya watu. Ni vyema wakashiriki kuelimisha,” anasema.
Polisi na takwimu za mauaji ya Dagashida
Takwimu za Jeshi la Polisi mkoani Simiyu zinaonyesha kuwa matukio ya mauaji hayo yanahusisha sababu mbalimbali ikiwamo kugombania mirathi, mipaka ya ardhi, imani za kishirikina pamoja na kujichukulia sheria mkononi.
Wiki iliyopita Mkuu wa Polisi Mkoa wa Simiyu Kamishna Msaidizi Salum Msangi alisema: “Nilipoingia Simiyu hali ilikuwa mbaya sana. Tulipokea ripoti za matukio kama hayo, hata ya watu watano kuuawa kwa siku, kuona hivyo kwa kushirikiana na mkuu wa mkoa tulizunguka Mkoa wa Simiyu wote kupiga marufuku uwepo wa baraza hilo…,”
Maelezo hayo ya Kamanda Msangi yalimaanisha kuwa katika kila siku saba za wiki watu 35 waliuawa mkoani Simiyu na katika mwezi mmoja wastani wa watu 150 waliuawa katika matukio yaliyohusisha kikundi cha Dagashida.
Hata hivyo, takwimu za jeshi hilo zilizotolewa wiki hii zinabainisha kwamba jumla ya watu 117 ameuawa katika vijiji mbalimbali vya Mkoa wa Simiyu kati ya Juni 2012 hadi Juni 2013.

Vifo hivyo ni wastani wa vifo vya wanakijiji 10 katika vijiji 12 vilivyo katika mkoa huo, ambao ulitokana na sehemu za Mkoa wa Shinyanga na ule wa Mwanza zilizomegwa na kuanzisha Mkoa wa Simiyu.
Akifafanua kuhusu mauaji hayo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Simiyu, Kamishna Msaidizi Salum Msangi anabainisha kuwa jeshi lake limewatia mbaroni watu 102 na kufikishwa katika vyombo vya sheria wakihusishwa na mauaji hayo.
Mauaji ya kishirikina
Idadi kubwa ya wakazi wa vijiji vya Simiyu wanakiri utekelezaji wa mauaji hufanywa na Baraza la Kimila la Dagashida, huku waathirika wakihusishwa na tuhuma za kishirikina.
Duru zinasema idadi kubwa ya waliouawa ni wanawake wakituhumiwa zaidi kuhusika na matukio ya kishirikina.
Kwa mujibu wa takwimu za Jeshi la Polisi, katika kipindi cha Juni 2012 hadi Juni 2013, wanakijiji 44 sawa na wastani wa watu watatu, waliuawa kila mwezi kwa tuhuma za ushirikina.Hata hivyo, Kamanda Msangi anasema kuwa rekodi za matukio ya kishirikina zinaonekana kupungua kwa kasi ukilinganisha na kipindi cha mwezi Juni mwaka jana.
“Juni mwaka jana wanakijiji 9 waliuawa ila kadri tunavyozidi kudhibiti, idadi inapungua na kwa mwezi Juni mwaka huu hakuna aliyeuawa kwa tuhuma za tukio kama hilo,” anasema.
Aliongeza kuwa mbali ya takwimu kuonyesha matumaini, hali bado siyo nzuri kwa baadhi ya vijiji hasa Wilaya ya Itilima.
“Huko ndiyo bado wanavichwa vigumu hawataki kubadilika, lakini tutahakikisha wanakoma,” anasema Kamanda Msangi.
Akichangia taarifa za mauaji hayo, Emmanuel Magunzagula mmoja wa wanakijiji wa Nyamiswi, Kata ya Gambushi, anasema kuwa kupitia Dagashida hilo, wamekuwa wakisadiki kuwa mwanamke pekee ndiyo mshirikina.
“Ukisikia mwanakijiji ameuawa kwa tuhuma za ushirikina basi atakuwa ni mwanamke, sijawahi kuona mwanamume ameuawa kwa tuhuma hizo hapa kijijini,” anasema Magunzagula na kuongeza: “Dhana hiyo inatokana na mfumo dume uliojengeka katika jamii.”
Anaongeza kuwa utekelezaji wa hukumu hizo unapofanyika, unaweza kusababisha familia yote kuuawa kwa mapanga.

“Mwanamke anayetuhumiwa anaweza kuuawa yeye na watoto wake wote, hawaangalii kama mtoto hana kosa, wao ni mapanga tu,” anasema Magunzagula.
Fisi wakoleza mauaji
Moja ya sababu kubwa inayotajwa kuchangia mauaji hayo ni wanakijiji wengi kupoteza maisha kwa kuliwa na mnyama fisi.
Chanzo chetu cha habari mkoani humo kinaeleza kuwa hadi sasa kuna matukio 40 ya wanakijiji kuliwa na fisi katika maeneo ya vijiji mbalimbali mkoani humo, huku jamii ikiamini kwamba mtu kuliwa na fisi hutokana na vitendo vya kishirikina.
“Kesi zipo, lakini hakuna ushahidi wa nani aliyehusika kwa sababu fisi wamezagaa sana mitaani, asubuhi saa moja unaweza kupishana na fisi, hivyo inaweza kuwa siyo ajabu watu kulia na fisi kutokana na mazingira hayo,” anasema Magunzagula.
Ugomvi wa mali na mipaka ya ardhi
Mauaji yatokanayo na ugomvi wa mipaka ya ardhi pia ni moja ya adha inayodaiwa kuwaathiri wanyonge tu katika mauaji hayo ya Dagashida.
Baraza la Dagashida limekuwa likituhumiwa kutumika kama silaha ya kulipiza kisasi miongoni mwa wanakijiji wanaogombania mipaka ya ardhi.
Takwimu za Jeshi la Polisi zinaonyesha kuwa katika mwaka mmoja uliopita (Juni 2012/13), wanakijiji 30 waliuawa wakati wakigombea mali, huku wengine 16 wakiuawa katika matukio ya watu kujichukulia sheria mkononi.
“Kwa hivyo ni wanakijiji 46 waliouawa ambao ni sawa na wastani wa wanakijiji wanne kila mwezi, hali hiyo bado ni mbaya. Lakini tunaendelea taratibu kuondoa changamoto hiyo kwa njia za kuelimisha na kuwachukulia hatua za kisheria,” anasema Kamanda Msangi.
Dini zinahitajika
Dini imetajwa kuwa moja kati ya njia kuu inayoweza kutumika kupunguza au kuondoa mila potofu zinazoshinikizwa na Dagashida.

Mwalimu wa Shule ya Sekondari ya Biashara iliyopo wilayani Bariadi, Emmanuel Bujiku anasema kuwa imani za dini zikienezwa ipasavyo Simiyu itasaidia jamii kumjua Mungu na kustaarabika.
“Watu wakiwa na imani za dini, iwe ya Kikristo au Kiislamu watakuwa wakiishi kwa hofu ya Mungu, hata mauaji haya yatapungua na kumalizika kabisa,” anasema Bujiku.
Kwa mujibu wa mazingira na uzoefu alionao mkoani humo, Bujiku anasema kuwa kwa sasa kati ya wanafunzi 50, watatu ndiyo wanajua dini. Akikiri hali hiyo, Kamanda Msangi anabainisha kuwa moja kati ya changamoto iliyopo maeneo mengi ya Mkoa wa Simiyu ni watu kutokuwa na imani za kidini.
“Hilo nalo ni tatizo, siyo wanakijiji tu, hata mwenyekiti au mtendaji wa kijiji hajui dini yoyote,” anasema.
Wabunge wa Simiyu
Kwa nyakati tofauti wananchi wa mkoa wa Simiyu wamewataka wabunge watano wa majimbo ya mkoa huo kushiriki katika harakati za kupambana na ukatili unayofanywa na Dagashida, wakiwataka pia viongozi wanaolitumia kisiasa baraza hilo kuacha mara moja.

Samaki hao kutoka Yemen, Dubai, China















 




Samaki


Afya za Watanzania ziko shakani kutokana na kuwapo kwa biashara ya kuingiza samaki kutoka nje ya nchi, wanaodaiwa kuharibika na kuuzwa katika la Soko la Feri jijini Dar es Salaam.
Samaki hao kutoka Yemen, Dubai, China na Japan, wanaoingizwa nchini wakiwa wameganda kwenye barafu, wengi huharibika muda mfupi baada ya barafu kuyeyuka au baada ya kununuliwa.

Uchunguzi wa gazeti hili umegundua kuwa samaki hao huletwa nchini kutafutiwa soko baada ya kukaa kwenye majokofu kwa muda mrefu huko wanakotoka, kiasi cha kuelekea kuharibika.

Ili wasiharibike, samaki hao aina ya Marckerel hukaangwa hadi wakauke. Uchunguzi zaidi umebaini kuwa wanunuzi wake wakuu ni wafanyabiashara wa chakula wakiwamo wamiliki wa migahawa na Mama Lishe wanaofanya shughuli zao katika miji ya Dar es Salaam, Pwani, Morogoro na Dodoma.

Samaki hao wanauzwa kwa bei ya chini ambayo ni Sh38,000 kwa boksi lenye uzito wa kilo 15, ikilinganishwa na wanaovuliwa hapa nchini ambao bei yake ni Sh60,000, kwa uzito huohuo.

Inaelezwa kuwa samaki hao baadhi yake ni wale ambao wamekwisha muda wake wa kutumika katika nchi hizo, hivyo kuingizwa nchini kutafutiwa soko.

Gazeti hili lilifika katika soko hilo kwa siku mbili na kushuhudia samaki hao wakiuzwa kwa wingi, huku wauzaji wakihimizwa wateja wao kuwahi kuwakaanga au kuwaweka kwenye jokofu.

Gazeti hili pia lilinunua boksi moja la samaki hao lenye uzito wa kilo 15 kwa Sh38,000, lakini lilipodai kupewa stakabadhi wauzaji walisema: “Hatuna stakabadhi ya kukupa ndugu yangu,” alisema muuzaji.

Baada ya kuwasafirisha kutoka Soko la Feri hadi ofisi za gazeti hili zilizopo Tabata Reli,


SAMAKI TISHIO KWA AFYA
Barabara ya Mandela kwa muda wa saa moja, tayari walikuwa wameharibika.

Baadhi ya samaki hao walianza kuoza huku wengine wakiwa wamelegea tofauti na samaki wa kawaida. Baada ya saa nne kupita, samaki hao waliharibika na kuanza kutoa harufu mbaya.

Dk Raymond Mwenekano wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, anayataja madhara ya ulaji wa samaki wa aina hiyo kuwa ni kupata magonjwa kama vile kansa ya utumbo, mwili kuwasha, kubabuka na vidonda mwilini.

“Madhara yake ni makubwa, ndiyo maana siku zote tunasisitiza kula vyakula visivyokaa sana kwani vingine vimehifadhiwa kwa dawa na wanaofanya hivi ni wafanyabiashara kwa faida yao,” alisema Dk Mwenekano.