Monday 23 September 2013

MASHAMBULIZI LA WESTGATE NAIROBI

Kenya
 
 
 
 
 
 
 
MASHAMBULIZI LA WESTGATE NAIROBI :
 Tanzania tunajiufunza nini? 
TUMEJIFUNZA NINI (3 photos)
Askari wakiwasaidia raia kujiokoa kwa kuwataka kutambaa badala ya kutembea wima au kukimbiaAskari mwenye silaha akiwaongoza watu waliofanikiwa kuokolewa kutoka kwenye jengo lililovamiwa na magaidi
Askari kanzu wakipambana ndani ya Westgate Mall katika harakati za kuwaokoa mateka
Matumizi mabaya yz siraha

Monday 16 September 2013

Serikali imeshindwa kudhibiti uhalifu wa tindikali nchini?


Namwaga lazi

Hujuma hii!
Matukio ya kumwagiwa tindikali yameendelea kukithiri huku Serikali ikiendelea kutoa ahadi za kudhibiti bila mafanikio.  Hivi karibuni baada ya raia wawili wa Uingereza kumwagiwa tindikali Zanzibar, Serikali iliweka mikakati mikali ya kudhibiti matumizi ya kemikali hiyo, lakini bado matukio hayo yameendelea kuwepo.
Tukio la kumwagiwa tindikali kwa Padri wa Kanisa Katoliki Parokia ya Cheju, Mkoa wa Kusini Unguja, Joseph Mwang’amba ni mwendelezo wa uhalifu huo ambao Serikali imeshindwa kabisa kuudhibiti.
Akieleza jinsi tukio hilo lilivyotokea, Padri Mwang’amba anasema alikuwa nje ya duka linalotoa huduma za mawasiliano ya mtandao (Sun Shine Internet Caffee) liliopo eneo la Mlandege Wilaya ya Mjini Unguja, ndipo alipotokea kijana mmoja na kumwagia tindikali.
Wakati Padri huyo akieleza hayo, Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, ameijia juu polisi kwa kushindwa kudhibiti matukio ya viongozi wa dini na Serikali visiwani humo, kushambuliwa kwa kumwagiwa tindikali huku akilitaka kuwakamata waliohusika na tukio hilo.
Kiongozi huyo wa dini, aliyejeruhiwa maeneo ya usoni, mikononi na kifuani baada ya kumwagiwa tindikali hiyo alisafirishwa jana na ndege ya kukodi ya Shirika la Coastal kutoka visiwani humo hadi Dar es Salaam na baadaye kupelekwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kwa matibabu zaidi.
Kwa upande wake, Padri wa Parokia ya Mtakatifu Joseph, Zanzibar, Thomas Assenga aliyefuatana na kiongozi huyo mpaka MNH, alisema siku za nyuma Padri Mwang’amba alitolewa vitisho na mtu ambaye hamfahamu wakati akienda kutoa huduma katika kituo cha wazee cha Welezo.
Alisema kabla ya kufika kituoni hapo, kuna eneo ambalo nyakati za asubuhi watu hufanya mazoezi barabarani ambapo kuna mtu mmoja alimtolea maneno ya vitisho.
Tukio hilo linafuatia tukio la Agosti 7, mwaka huu ambapo raia wawili wa Uingereza, Kate Gee (18) na Kirstie Trup (18) walimwagiwa tindikali katika maeneo ya Mji Mkongwe, Zanzibar na vijana wawili waliokuwa wakiendesha pikipiki aina ya Vespa.
Waingereza hao walisafirishwa siku tatu baadaye kurudi kwao Uingereza kwa ajili ya matibabu.
Utetezi wa Serikali
Siku tano baada ya tukio la Waingereza hao kumwagiwa tindikali, Serikali kupitia vyombo vyake vya uchunguzi iliwataka wananchi kuisaidia kuwafichua na kutoa ushahidi wa uhalifu huo kwani ni vigumu kuwabaini wahusika.
Kauli hiyo ilitolewa kwa pamoja jana na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Said Mwema, Mkemia Mkuu wa Serikali, Profesa Samwel Manyele na Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali (DPP) Eliezer Feleshi, katika mkutano wao na waandishi wa habari, uliolenga kueleza mikakati ya kupambana na matumizi yasiyo sahihi ya tindikali nchini.
 Mkemia Mkuu, Polisi hawawezi kubaini matukio haya bila ushirikiano wa wananchi kwani Tanzania ni nchi kubwa na ina watu zaidi ya milioni 45. Watu wanaingiza tindikali lakini wapo ambao wanatumia tindikali hiyo kwa matumizi haramu,” alisema IGP Mwema.
Amesema tindikali inaweza kutolewa kwa ajili ya shughuli za viwandani, maabara na usafirishaji na kwamba watu wanapotaka kuitumia kwa ajili ya kufanya uovu wanaweza kugundulika kupitia kwa taarifa zitakazotolewa na wananchi, kwa sababu wanakuwa wamezungukwa na jamii ya watu mbalimbali.
Matukio mengine
Tukio lingine lililoshtua ni lile la bilionea Said Mohamed Saad ambaye ni mmiliki wa maduka ya Home Shopping Centre, kumwagiwa tindikali mwanzoni mwa mwezi Agosti.
Said anaendelea na matibabu nchini Afrika Kusini na inaelezwa kuathirika vibaya usoni, mikononi na kifuani.
Alimwagiwa tindikali Julai 19, mwaka huu akiwa kwenye moja ya maduka yake katika Jengo la Msasani Mall, Dar es Salaam.
Taarifa za siku ya tukio zilibainisha kuwa Said alikuwa akizungumza na mfanyakazi wake muda wa saa moja jioni ndipo akatokea kijana mrefu, mwembamba ambaye alimmwagia kimiminika kinachosadikiwa kuwa ni tindikali.
Ilibainishwa kwamba mfanyakazi huyo wa Said, Hassan Ahmad naye alijeruhiwa kidogo katika purukushani hiyo lakini alipopelekwa Hospitali ya Ami Wellness Centre, alitibiwa na kuruhusiwa huku bosi wake akipelekwa Afrika Kusini usiku huohuo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camilius Wambura anasema matukio ya kutumia pikipiki yanaonyesha kupangwa hivyo inakuwa vigumu kuwabaini wahalifu mapema. 
Tukio hilo linafanana na lile lililotokea Septemba 8, mwaka huu ambapo mfanyabiashara wa vifaa vya ujenzi, Christian Msema wa Mburahati jijini Dar es Salaam, alimwagiwa kemikali hiyo na watu waliokuwa kwenye pikipiki ya matairi matatu.
Msema maarufu kama Mnyalu amelihusisha tukio hilo lilitokea jioni ya Jumamosi Septemba 8 na mgogoro wa eneo la wazi ambapo yeye alikuwa akipinga mfanyabiashara mmoja (jina linahifadhiwa) kulitumia kuegesha magari yake.
Akizungumza kwa shida katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili alikolazwa anakiri kuwa mstari wa mbele kupinga eneo hilo kutumiwa kinyume na sheria.

“Awali vijana wasio na ajira waliomba eneo hilo ili walitumie kwa mradi wa kuegesha magari, wakaandika barua, lakini Serikali ya mtaa ikakataa ikisema hilo ni eneo la kazi. Hiyo ilikuwa mwezi Oktoba mwaka jana, ilipofika Novemva, tukaona malori yanaegeshwa pale. Tulipofuatilia tukaambiwa ni mwenyekiti wa mtaa ameruhusu,” anasema na kuongeza:
“Tukajiorodhesha wana mtaa tukafika kama watu 60 na mimi nikawa mwenyekiti wao, tukapeleka barua yetu kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni ambaye aliipeleka kwa ofisa wa mipango miji.”
Ameongeza kuwa ofisi ya mipango miji ya Kinondoni ilisema hilo ni eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa shule ya sekondari hivyo ikaagizwa kuwa magari hayo yaondolewe. 
“Kampuni iliyopewa tenda ya kuondoa yale magari ilifanya kazi bila kutoa notisi, ndipo yule mwenye magari akaenda kulalamika kwa mkuu wa mkoa. Malalamiko yakafika kwa Mkurugenzi ambaye aliagiza kampuni hiyo irejeshe hayo magari ili utaratibu ufuatwe,” alisema.  Aliendelea kusema kuwa yule mfanyabiashara aliendelea kukaidi kwa kuongeza magari mengine kwenye uwanja huo hadi yalipokuja kuondolewa kwa nguvu.
Msema alisema wakati mvutano huo ukiendelea, aliwahi kukutana na mlinzi wa mfanyabiashara huyo ambaye alimtahadharisha kuwa harakati zake hizo zitamponza kwani anafuatiliwa.
“Mimi sikukata tamaa kwani lile ni eneo la umma kwa nini mtu ang’ang’anie? Lakini watu wengi walinitahadharisha kuwa yule jamaa ananifuatilia, ndiyo maana siku ile ya tukio kuna bajaji kumbe ilikuwa inanifuatilia kwa muda mrefu,” anasema.
Mwenyekiti wa mtaa wa Mburahati, Tungaraza amekanusha kuwepo kwa mgogoro huo huku akimtaka mwandishi afike ofisini kwake kwanza.  Matukio  hayo yameanza muda mrefu na wakati mwingine yamehusishwa na chuki za kisiasa.
Baadhi ya wananchi wanashauri Serikali kuwa imara na tindikali hasa katika chaguzi zijazo, kwani tindikali ni rahisi kuibeba.

twiga

Sunday 15 September 2013

Dawa ya mifugo yatengenezea gongo Dar

Dar es Salaam. Wakati Serikali ikiahidi kuongeza nguvu katika vita dhidi ya wauza dawa za kulevya nchini,
imebainika kuwa kuna mtandao wa wafanyabiashara wa pombe haramu ya gongo unaopika na kuichanganya na dawa za mifugo ili kuiongezea ukali.
Mtandao huo unaomiliki mitambo ya kupika gongo katika eneo la Mto Kizinga uliopo Dambweni, Kata ya Kilungule, wilayani Temeke, unadaiwa kuchanganya pombe hiyo na dawa ya mifugo aina ya Multivitamin ambayo hutumika kurutubisha wanyama.
Hata hivyo, uchunguzi uliofanywa na gazeti hili umebaini kuwa dawa hiyo huchanganywa na dawa nyingine ambayo haikufahamika mara moja, kisha kuiweka kwenye gongo ili kuiongezea ukali zaidi.
Wafanyabiashara hao wamekuwa wakipika gongo hiyo katika eneo hilo kwa miaka zaidi ya 10, huku baadhi ya viongozi wa serikali ya mtaa wakitajwa kuwalinda.
Kwa mujibu wa uchunguzi, eneo hilo lina mitambo zaidi ya minne ya kutengeneza gongo na kila mtambo unazalisha pipa moja lenye ujazo wa lita 200.
Mtambo wa gongo
Uchunguzi ulibaini kuwa kila siku wanazalisha zaidi ya lita 800 za gongo ambayo huuzwa kwa rejareja na jumla. Bei ya rejareja kipimo kinaanzia Sh500 hadi Sh5,000, ambapo bei ya jumla ni Sh38,000 kwa ndoo yenye ujazo wa lita 20.
Kwa mtu anayefika kwa mara ya kwanza eneo hilo atakutana na makundi ya watu wakiwa chini ya miti wakijipumzisha wakati wakisubiri pombe hiyo kuwa tayari, huku wakazi wengine wa eneo hilo wakionekana kuendelea na shughuli zao kwenye bustani za mboga za majani zilizolimwa kando kando ya mto.
Mbali ya kuwa wanalindwa na baadhi ya viongozi wa mtaa, wameweka ulinzi wao wenyewe, kwa kuweka vijana zaidi ya 10 ambao hukaa katika eneo hilo kuhakikisha kuwa mtu anayefika katika eneo hilo wanamtambua.
Ukifika katika eneo ilipo mitambo yao, watu wanaofanya kazi ya kupika ni wacheshi, wanaojaribu kumsalimia kila mpita njia bila ya kuwa na hofu yoyote, huku mmojawao ambaye jina lake halikufahamika mara moja akisema kuwa wao ndio waliotengeneza barabara ya kupita magari inayoingia sehemu hiyo.
Mkazi mmoja wa eneo hilo ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini kwa kuhofia usalama wake, alisema watu hao ndiyo wasambazaji wakubwa wa gongo jijini Dar es Salaam.
“Biashara hii inalipiwa ‘kodi’ kila mwezi, hawa jamaa huchangishana fedha halafu huwapelekea baadhi ya askari ambao huwalinda wasikamatwe, kuna wakati huchanga hadi laki tatu. Vigumu sana kukamatwa,” alisema.
Gongo inavyotengenezwa

Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili ulibaini pombe hiyo inatengenezwa kwa kutumia malighafi mbalimbali ikiwamo mapapai yaliyooza, vitambaa vichafu vilivyovunda, mihogo na wakati mwingine kinyesi cha binadamu hasa wakati bidhaa nyingine zinapoadimika.
Mfanyabiashara mmoja (jina linahifadhiwa) alisema amekuwa akipika gongo na kuigawa katika madaraja matatu; iliyopikwa kwa mapapai yaliyooza ndiyo inayopendwa zaidi na wateja wake ikilinganishwa na iliyotumia malighafi nyingine.
“Sisi tunatumia mapapai yaliyooza, tunaongeza na sukari pamoja na hamira, ikishaiva tunaitenga kutokana na madaraja yake. Gongo ya eneo hili inasifika sana kwa sababu ya ubora wake, hatuna tatizo la ukosefu wa maji kama walilonalo wenzetu ndiyo maana unaona tunaung’ang’ania huu mto hapa,” alisema na kuongeza :
“Kama mapapai yakiadimika sana, tunaweza kupika kwa kutumia vitambaa vichafu au mihogo.”
Akifafanua alisema wamekuwa wakitembea kwenye madampo kuokota vitambaa pamoja na takataka nyingine, kisha huziloweka kwenye maji kwa muda mrefu hadi zivunde ndipo huwa tayari kwa kupikia gongo.
Uchunguzi uliofanywa unaonyesha kuwa mbali ya pombe hiyo kutengenezwa kwa kutumia takataka zinazookotwa kwenye madampo, pia huongezewa ukali kwa kutumia dawa za kuongezea vitamini mifugo.
Mteja mmoja wa pombe hiyo ambaye alijitambulisha kwa jina moja la Sadick, alisema gongo inayopikwa eneo hilo imekuwa maarufu kwa kuwa kuna dawa ya mifugo ya Multivitamin ambayo huongezwa baada ya pombe hiyo kuiva.
“Mimi ninafahamu kuna dawa ya mifugo inawekwa kwenye hii gongo ili kuiongezea nguvu. Sijui ni dawa aina gani, lakini kuna jamaa huwa namwona anakuja kuuza hiyo dawa. Gongo iliyowekwa hiyo dawa inakuwa na nguvu sana,”alisema Sadick.
Mtaalamu wa Mifugo, Joseph Nong’ona alisema wanywaji wa pombe hiyo wapo katika hatari ya kudhurika kiafya kwa kuwa dawa ya Multivitamin inayotolewa kwa wanyama ina nguvu zaidi ikilinganishwa na ya binadamu, na kwamba mtu haruhusiwi kunywa maziwa au nyama ya mnyama aliyepewa dawa hiyo kwa siku tatu.
“Multivitamin anayopewa mnyama ina ‘concentration’ kubwa ikilinganishwa na ile ya binadamu, lakini pia ikumbukwe kuwa ile ni kemikali sijui inakuwaje inapochanganywa na gongo ambayo yenyewe tu ina madhara makubwa kiafya. Kwa kawaida mnyama akipewa dawa hiyo huwa tunashauri asikamuliwe mazima au nyama yake isitumike kwa siku tatu,” alisema Nong’ona.
Akizungumzia biashara hiyo, Katibu wa Mtaa wa Kilungule, Juma Ahmed aliwatetea wafanyabiashara hao kwa madai kuwa hajawahi kupata taarifa zozote za kufanya uhalifu badala yake wamekuwa walinzi wa amani katika mtaa huo.“Ni watu wazuri sana, sijawahi kusikia wamefanya jambo lolote baya, kwanza wamegeuka kuwa walinzi wa amani hapa mtaani kwetu… wanajua biashara wanayoifanya siyo halali kwa hiyo hawataki matatizo na mtu,” alisema Ahmed.
Kamanda wa Polisi wa Temeke, Engelbert Kiondo alisema suala la biashara ya gongo linatakiwa kudhibitiwa na jamii inayowazunguka wafanyabishara hao kwa kutumia ulinzi shirikishi.

“Wanataka kuipa Polisi kazi bure tu, jamii ndiyo inayohusika na suala hilo. Serikali ya mtaa kwa njia ya ulinzi shirikishi wanaweza kuamua kwenda kuvunja mitambo ya gongo,” alisema Kiondo.
Akizungumzia tuhuma kuwa baadhi ya Polisi wanawalinda wafanyabiashara wa gongo, Kiondo alisema tuhuma hizo zimekuwepo muda mrefu na kwamba zimeshapitwa na wakati.

Polisi Simiyu yatoa ripoti ukatili wa Dagashida, fisi wakoleza mauaji



Wiki iliyopita katika ukurasa huu, tuliwaletea mwendelezo wa ripoti maalumu kuhusu mauaji yaliyokuwa yakitekelezwa mkoani Simiyu kupitia Baraza la Kimila maarufu Dagashida na jinsi wananchi wanavyoogopa kutoa ushirikiano kwa polisi.
Leo tunaendelea na sehemu ya tatu na ya mwisho ya ripoti hiyo, pamoja na mambo mengine ikiainisha takwimu za vifo zilizotolewa na Jeshi la Polisi kutokana na matukio mbalimbali ya mauaji ya Dagashida.
Wanakijiji hawatoi ushirikiano
Kamanda Msangi anakiri kuwepo kwa changamoto ya kukosa ushirikiano kutoka kwa wananchi wakihofia usalama wao.
“Sisi tunawaomba wasiogope kutoa taarifa za ukatili huo, lakini pia tunaomba mashirika na dini waendelee kuelimisha,”anasema Kamanda Msangi.
Anaeleza kusikitishwa kwake na viongozi wa kisiasa kutoshiriki katika harakati za kukemea ukatili wa baraza hilo akifafanua tangu alipoanza kazi mkoani Simiyu hajawahi kuona wala kusikia mbunge yeyote wa mkoa huo akikemea ukatili wa Dagashida.
“Hakuna mbunge au diwani yeyote mwenye nguvu ya kuzuia baraza hilo kwa sababu wanalitumia kisiasa, kwa hivyo niwaombe waache kuchanganya siasa na maisha ya watu. Ni vyema wakashiriki kuelimisha,” anasema.
Polisi na takwimu za mauaji ya Dagashida
Takwimu za Jeshi la Polisi mkoani Simiyu zinaonyesha kuwa matukio ya mauaji hayo yanahusisha sababu mbalimbali ikiwamo kugombania mirathi, mipaka ya ardhi, imani za kishirikina pamoja na kujichukulia sheria mkononi.
Wiki iliyopita Mkuu wa Polisi Mkoa wa Simiyu Kamishna Msaidizi Salum Msangi alisema: “Nilipoingia Simiyu hali ilikuwa mbaya sana. Tulipokea ripoti za matukio kama hayo, hata ya watu watano kuuawa kwa siku, kuona hivyo kwa kushirikiana na mkuu wa mkoa tulizunguka Mkoa wa Simiyu wote kupiga marufuku uwepo wa baraza hilo…,”
Maelezo hayo ya Kamanda Msangi yalimaanisha kuwa katika kila siku saba za wiki watu 35 waliuawa mkoani Simiyu na katika mwezi mmoja wastani wa watu 150 waliuawa katika matukio yaliyohusisha kikundi cha Dagashida.
Hata hivyo, takwimu za jeshi hilo zilizotolewa wiki hii zinabainisha kwamba jumla ya watu 117 ameuawa katika vijiji mbalimbali vya Mkoa wa Simiyu kati ya Juni 2012 hadi Juni 2013.

Vifo hivyo ni wastani wa vifo vya wanakijiji 10 katika vijiji 12 vilivyo katika mkoa huo, ambao ulitokana na sehemu za Mkoa wa Shinyanga na ule wa Mwanza zilizomegwa na kuanzisha Mkoa wa Simiyu.
Akifafanua kuhusu mauaji hayo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Simiyu, Kamishna Msaidizi Salum Msangi anabainisha kuwa jeshi lake limewatia mbaroni watu 102 na kufikishwa katika vyombo vya sheria wakihusishwa na mauaji hayo.
Mauaji ya kishirikina
Idadi kubwa ya wakazi wa vijiji vya Simiyu wanakiri utekelezaji wa mauaji hufanywa na Baraza la Kimila la Dagashida, huku waathirika wakihusishwa na tuhuma za kishirikina.
Duru zinasema idadi kubwa ya waliouawa ni wanawake wakituhumiwa zaidi kuhusika na matukio ya kishirikina.
Kwa mujibu wa takwimu za Jeshi la Polisi, katika kipindi cha Juni 2012 hadi Juni 2013, wanakijiji 44 sawa na wastani wa watu watatu, waliuawa kila mwezi kwa tuhuma za ushirikina.Hata hivyo, Kamanda Msangi anasema kuwa rekodi za matukio ya kishirikina zinaonekana kupungua kwa kasi ukilinganisha na kipindi cha mwezi Juni mwaka jana.
“Juni mwaka jana wanakijiji 9 waliuawa ila kadri tunavyozidi kudhibiti, idadi inapungua na kwa mwezi Juni mwaka huu hakuna aliyeuawa kwa tuhuma za tukio kama hilo,” anasema.
Aliongeza kuwa mbali ya takwimu kuonyesha matumaini, hali bado siyo nzuri kwa baadhi ya vijiji hasa Wilaya ya Itilima.
“Huko ndiyo bado wanavichwa vigumu hawataki kubadilika, lakini tutahakikisha wanakoma,” anasema Kamanda Msangi.
Akichangia taarifa za mauaji hayo, Emmanuel Magunzagula mmoja wa wanakijiji wa Nyamiswi, Kata ya Gambushi, anasema kuwa kupitia Dagashida hilo, wamekuwa wakisadiki kuwa mwanamke pekee ndiyo mshirikina.
“Ukisikia mwanakijiji ameuawa kwa tuhuma za ushirikina basi atakuwa ni mwanamke, sijawahi kuona mwanamume ameuawa kwa tuhuma hizo hapa kijijini,” anasema Magunzagula na kuongeza: “Dhana hiyo inatokana na mfumo dume uliojengeka katika jamii.”
Anaongeza kuwa utekelezaji wa hukumu hizo unapofanyika, unaweza kusababisha familia yote kuuawa kwa mapanga.

“Mwanamke anayetuhumiwa anaweza kuuawa yeye na watoto wake wote, hawaangalii kama mtoto hana kosa, wao ni mapanga tu,” anasema Magunzagula.
Fisi wakoleza mauaji
Moja ya sababu kubwa inayotajwa kuchangia mauaji hayo ni wanakijiji wengi kupoteza maisha kwa kuliwa na mnyama fisi.
Chanzo chetu cha habari mkoani humo kinaeleza kuwa hadi sasa kuna matukio 40 ya wanakijiji kuliwa na fisi katika maeneo ya vijiji mbalimbali mkoani humo, huku jamii ikiamini kwamba mtu kuliwa na fisi hutokana na vitendo vya kishirikina.
“Kesi zipo, lakini hakuna ushahidi wa nani aliyehusika kwa sababu fisi wamezagaa sana mitaani, asubuhi saa moja unaweza kupishana na fisi, hivyo inaweza kuwa siyo ajabu watu kulia na fisi kutokana na mazingira hayo,” anasema Magunzagula.
Ugomvi wa mali na mipaka ya ardhi
Mauaji yatokanayo na ugomvi wa mipaka ya ardhi pia ni moja ya adha inayodaiwa kuwaathiri wanyonge tu katika mauaji hayo ya Dagashida.
Baraza la Dagashida limekuwa likituhumiwa kutumika kama silaha ya kulipiza kisasi miongoni mwa wanakijiji wanaogombania mipaka ya ardhi.
Takwimu za Jeshi la Polisi zinaonyesha kuwa katika mwaka mmoja uliopita (Juni 2012/13), wanakijiji 30 waliuawa wakati wakigombea mali, huku wengine 16 wakiuawa katika matukio ya watu kujichukulia sheria mkononi.
“Kwa hivyo ni wanakijiji 46 waliouawa ambao ni sawa na wastani wa wanakijiji wanne kila mwezi, hali hiyo bado ni mbaya. Lakini tunaendelea taratibu kuondoa changamoto hiyo kwa njia za kuelimisha na kuwachukulia hatua za kisheria,” anasema Kamanda Msangi.
Dini zinahitajika
Dini imetajwa kuwa moja kati ya njia kuu inayoweza kutumika kupunguza au kuondoa mila potofu zinazoshinikizwa na Dagashida.

Mwalimu wa Shule ya Sekondari ya Biashara iliyopo wilayani Bariadi, Emmanuel Bujiku anasema kuwa imani za dini zikienezwa ipasavyo Simiyu itasaidia jamii kumjua Mungu na kustaarabika.
“Watu wakiwa na imani za dini, iwe ya Kikristo au Kiislamu watakuwa wakiishi kwa hofu ya Mungu, hata mauaji haya yatapungua na kumalizika kabisa,” anasema Bujiku.
Kwa mujibu wa mazingira na uzoefu alionao mkoani humo, Bujiku anasema kuwa kwa sasa kati ya wanafunzi 50, watatu ndiyo wanajua dini. Akikiri hali hiyo, Kamanda Msangi anabainisha kuwa moja kati ya changamoto iliyopo maeneo mengi ya Mkoa wa Simiyu ni watu kutokuwa na imani za kidini.
“Hilo nalo ni tatizo, siyo wanakijiji tu, hata mwenyekiti au mtendaji wa kijiji hajui dini yoyote,” anasema.
Wabunge wa Simiyu
Kwa nyakati tofauti wananchi wa mkoa wa Simiyu wamewataka wabunge watano wa majimbo ya mkoa huo kushiriki katika harakati za kupambana na ukatili unayofanywa na Dagashida, wakiwataka pia viongozi wanaolitumia kisiasa baraza hilo kuacha mara moja.

Samaki hao kutoka Yemen, Dubai, China















 




Samaki


Afya za Watanzania ziko shakani kutokana na kuwapo kwa biashara ya kuingiza samaki kutoka nje ya nchi, wanaodaiwa kuharibika na kuuzwa katika la Soko la Feri jijini Dar es Salaam.
Samaki hao kutoka Yemen, Dubai, China na Japan, wanaoingizwa nchini wakiwa wameganda kwenye barafu, wengi huharibika muda mfupi baada ya barafu kuyeyuka au baada ya kununuliwa.

Uchunguzi wa gazeti hili umegundua kuwa samaki hao huletwa nchini kutafutiwa soko baada ya kukaa kwenye majokofu kwa muda mrefu huko wanakotoka, kiasi cha kuelekea kuharibika.

Ili wasiharibike, samaki hao aina ya Marckerel hukaangwa hadi wakauke. Uchunguzi zaidi umebaini kuwa wanunuzi wake wakuu ni wafanyabiashara wa chakula wakiwamo wamiliki wa migahawa na Mama Lishe wanaofanya shughuli zao katika miji ya Dar es Salaam, Pwani, Morogoro na Dodoma.

Samaki hao wanauzwa kwa bei ya chini ambayo ni Sh38,000 kwa boksi lenye uzito wa kilo 15, ikilinganishwa na wanaovuliwa hapa nchini ambao bei yake ni Sh60,000, kwa uzito huohuo.

Inaelezwa kuwa samaki hao baadhi yake ni wale ambao wamekwisha muda wake wa kutumika katika nchi hizo, hivyo kuingizwa nchini kutafutiwa soko.

Gazeti hili lilifika katika soko hilo kwa siku mbili na kushuhudia samaki hao wakiuzwa kwa wingi, huku wauzaji wakihimizwa wateja wao kuwahi kuwakaanga au kuwaweka kwenye jokofu.

Gazeti hili pia lilinunua boksi moja la samaki hao lenye uzito wa kilo 15 kwa Sh38,000, lakini lilipodai kupewa stakabadhi wauzaji walisema: “Hatuna stakabadhi ya kukupa ndugu yangu,” alisema muuzaji.

Baada ya kuwasafirisha kutoka Soko la Feri hadi ofisi za gazeti hili zilizopo Tabata Reli,


SAMAKI TISHIO KWA AFYA
Barabara ya Mandela kwa muda wa saa moja, tayari walikuwa wameharibika.

Baadhi ya samaki hao walianza kuoza huku wengine wakiwa wamelegea tofauti na samaki wa kawaida. Baada ya saa nne kupita, samaki hao waliharibika na kuanza kutoa harufu mbaya.

Dk Raymond Mwenekano wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, anayataja madhara ya ulaji wa samaki wa aina hiyo kuwa ni kupata magonjwa kama vile kansa ya utumbo, mwili kuwasha, kubabuka na vidonda mwilini.

“Madhara yake ni makubwa, ndiyo maana siku zote tunasisitiza kula vyakula visivyokaa sana kwani vingine vimehifadhiwa kwa dawa na wanaofanya hivi ni wafanyabiashara kwa faida yao,” alisema Dk Mwenekano.

LOWASSA AWA MLEZI WA MACHIFU



 
 
 
 
 
 
 
 
 
LOWASSA AWA MLEZI WA MACHIFU

Pichani : Chifu Msagati Ngulyati Saidi Fundikira akimsimika rasmi Waziri Mkuu aliyejiuzulu, ambaye pia ni Mbunge wa Monduli, Mh. Edward Lowassa, kuwa mlezi wa machifu wa Tanzania. 

Hafla hii ilifanyika katika Ikulu ya Unyanyembe Kipalapala.Pichani : Chifu Msagati Ngulyati Saidi Fundikira akimsimika rasmi Waziri Mkuu aliyejiuzulu, ambaye pia ni Mbunge wa Monduli, Mh. Edward Lowassa, kuwa mlezi wa machifu wa Tanzania.

Hafla hii ilifanyika katika Ikulu ya Unyanyembe Kipalapala.

MIMI NASEMA HAPANA....

Zigua Samba, Bondei
wana maombi
Maneno ya mungu
Mini nasema hapana yanayotokea Zanzibar yasihusishwa na imani za kiroho ...lakini nikwasababu gani niseme hivi sisi wakristi, na sisi waislami sisi wite ni watoto wa baba mmoja na mama mmoja si ajabu hivi sasa kumuona Mkristu ao mweislami kutinga (kuingia katuka nyumba za ibada na si ajabu kwa mwislamu kusikika akiimba nyimbo za mapambio za kujifariji au za kujipa moyo....si hilotuu lakini tisiishie hapo hata tukiona yakuwa Mkristu kusimama na ndugu zao wa islamu huku akitamka SALAM-ALEIKUM bila ya ajizi hii ni kutokana na undugu wetu ulio shibika tangu miaka ya Mhela mwana, (miongo ya kale) na si hilo tuu bali pia Ndoa, Mazishi, Shughili za maendeleo, shughuli za kusiasa....Tuna vyama vya kisiasa, vyama michezo, hata vyama vya upatu, vyote hutoona ubaguzi baina ya Wakristu na waislamu...haya katika vyombo vya usafiri, katika Maofisi Nikipandishwa cheo hata sikumoja sijawahi kumsikia aidha Mwislamu, Mkristu, au Mpagani atafumgua mdomo wake na kudai kwanini huyo mwenzangu apendelewe ....LAKINI HEBU TUJIULIZENI HIVI KULIKONI??????

sisi wananchi kwa umoja weto tunapaswa kukikemea kitendo hiki cha kijasusi kinacho endelea cha kuwaangamiaza viongozi wetu wa kiroho bila ya kujali yakuwa awe Mkristu, Mwislamu, Nahata, awe Mpagani kwa pamoja tuwekeni msisitizo kuhusiana na kuwatesa hawa watu wa mungu!!

Kwamana hiyo uma wa watanzania nilazima tupambane na kikundi hiki au vikundi hivi vinavya lenga kutugawa sisi, nyinyi, na hata wao

 "TUWENI NA MSHIKA MANO KUWABAINI WANAO UZA WANAO NUNUA NA WALE WANAO TUMWA KUTENDA UHALIFU DHIDI YA WATU WETU WASIO NA HATIA......"

TUNDI KALI: (Tunaomba serikali ipige marufuku bidhaa hii haraka iwezekazavyo kama madawa ya kulevya)...na atakae bainika kuwa nayo basi vyombo vya ulinzi na usalama vimchukulie hatua..

 BILA YA KUMUONEA AIBU.....Tunatoa pole kwa viongozo wetu wote wa kiroho awe wakikristu au wa kiislamu na hata wa kipagani wafanye kazi zao bila ya kuogopa na walione swala hili ya kuwa ni moja ya changamoto katuka kuifanya kazi zao.

TUNA WASILISHA TAARIFA YA KIONGOZI WA KIROHO...NA YALIYO MSIBU.

"
  • PADRI ALITISHIWA KUUAWA KABLA HAJAMWAGIWA TINDIKALI

     
     
     
     
    Maadili ya kidini
    PADRI ALITISHIWA KUUAWA KABLA HAJAMWAGIWA TINDIKALI

Padri wa Kanisa Katoliki Parokia ya Cheju, Mkoa wa Kusini Unguja, Joseph Mwang’amba, aliyejeruhuiwa maeneo ya usoni, mikononi na kifuani baada ya kumwagiwa tindikali na watu wasiojulikana, alitoa polisi kiasi cha miezi mitatu iliyopita kuwa alikuwa anatishiwa usalama wa maisha yake.

Akitoa taarifa hizi, Padri wa Parokia ya Mtakatifu Joseph, Zanzibar, Thomas Assenga alisema siku za nyuma Padri Mwang’amba alitolewa vitisho na mtu ambaye hamfahamu wakati akienda kutoa huduma katika kituo cha wazee cha Welezo.

“Unajua kawaida ya watu wa Zanzibar hufanya mazoezi barabarani, sasa kipindi anapita eneo hilo katika kilima, kuna mtu alimwambia atamfanyia kitu kibaya ambacho hatujui ndiyo hiki au la,” alisema Padri Assenga na kuongeza kuwa “mara baada ya kupewa vitisho hivyo alikwenda kutoa taarifa kwa Sheha wa eneo hilo na kituo cha polisi.”

PICHANI : Padri Mwang'amba akishuka kutoka kwenye ndege ya kukodi iliyomsafirisha kutoka Zanzibar kuja Dar es Salaam kwa matibabu zaidi katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH)
    Kiongozi w kiroho
    Padri wa Kanisa Katoliki Parokia ya Cheju, Mkoa wa Kusini Unguja, Joseph Mwang’amba, aliyejeruhuiwa maeneo ya usoni, mikononi na kifuani baada ya kumwagiwa tindikali na watu wasiojulikana, alitoa polisi kiasi cha miezi mitatu iliyopita kuwa alikuwa anatishiwa usalama wa maisha yake.

    Akitoa taarifa hizi, Padri wa Parokia ya Mtakatifu Joseph, Zanzibar, Thomas Assenga alisema siku za nyuma Padri Mwang’amba alitolewa vitisho na mtu ambaye hamfahamu wakati akienda kutoa huduma katika kituo cha wazee cha Welezo.

    “Unajua kawaida ya watu wa Zanzibar hufanya mazoezi barabarani, sasa kipindi anapita eneo hilo katika kilima, kuna mtu alimwambia atamfanyia kitu kibaya ambacho hatujui ndiyo hiki au la,” alisema Padri Assenga na kuongeza kuwa “mara baada ya kupewa vitisho hivyo alikwenda kutoa taarifa kwa Sheha wa eneo hilo na kituo cha polisi.”

    PICHANI : Padri Mwang'amba akishuka kutoka kwenye ndege ya kukodi iliyomsafirisha kutoka Zanzibar kuja Dar es Salaam kwa matibabu zaidi katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH)
    Kazi ya Mungu
     

Saturday 14 September 2013

Hatutavumilia wahamiaji haramu

Tanzania: Hatutavumilia 

wahamiaji haramu

Tanzania: Hatutavumilia wahamiaji haramuWizara ya Mambo ya Ndani ya nchini Tanzania imetoa tamko kwa wahamiaji haramu kurejea makwao mara moja kwa hiyari, kwani zoezi la kuwasaka na kuwarejesha litaanza wakati wowote kuanzia sasa. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk. Emmanuel Nchimbi amesema tayari amekabidhiwa na Rais Jakaya Kikwete jukumu la kuwahamisha wahamiaji haramu waliopo katika mikoa ya Kagera, Kigoma na Geita. Kauli hiyo ya Dk. Nchimbi imekuja baada ya wiki mbili alizotoa Rais Jakaya Kikwete kwa wahamiaji hao kumalizika. Rais Kikwete alipokuwa mkoani Kagera Julai 29 mwaka huu, alitoa tamko kwa wahamiaji wote haramu waliopo katika mkoa huo na maeneo jirani kufunga virago na kurejea makwao. Wahamiaji hao haramu waliorejea makwao ni kutoka nchi za Rwanda, Burundi, Uganda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Dk. Nchimbi  amesema, wakati wa wahamiaji haramu kurejea makwao ni sasa, kwani Tanzania haitavumilia tena wahamiaji haramu.  Ameongeza kuwa, wahamiaji haramu wanaotaka kuishi Tanzania warejee makwao, kisha wafuate taratibu za kuingia na kuishi Tanzania.

Andika maoni







Msimbo salama (Security code)
Upyesha (Refresh)


M23 wameahidi kuendeleza mapambano ikiwa leo hawatafikia makubaliano








M.23
Wawakilishi wa kundi la upinzani la  M23 wanatazamiwa kukutana na maofisa wa Serikali ya Kinshasa leo  katika mji mku wa Uganda, Kampala kwa lengo la kujadili njia za kumaliza mapigano mashariki mwa Kongo.
Rais Kabila alisema juhudi zitafanyika kufanikisha mazungumzo ya Kampala lakini alionya kuwa iwapo mazungumzo hayo hayatafanikiwa jeshi litaendeleza oparesheni dhidi ya waasi.
Juzi Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo alifungua
mazungumzo ya maelewano ya kitaifa ambayo yanawashirikisha wapinzani na makundi ya kijamii.
Katika ufunguzi wa kikao hicho cha wiki mbili viongozi kadhaa wa upinzani hawakushiriki huku wakimtuhumu Kabila kuwa anapanga kutawala kwa muhula wa tatu mfululizo kinyume cha sheria.
Kabila ambaye muhula wake unamalizika mwaka 2016 alisema mazungumzo hayo yanalenga kujadili sababu za kudhoofika utendaji kazi wa taasisi za kiserikali, pamoja na mapigano Mashariki mwa nchi hiyo ambayo yalianzishwa na wapinzani wa M23miezi 18 iliyopita.
Mazungumzo hayo ya kitaifa ambayo yalipangwa kuanza mwezi Novemba mwaka jana yalianza katika hali ambayo Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imepata mafanikio makubwa katika mapambano dhidi ya wapinzani.
Mafanikio hayo yalipatikana kutokana na uungaji mkono wa kikosi cha uingiliaji cha Umoja wa Mataifa.
Wito uliotolewa na viongozi wa nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu wa kuitaka Serikali ya Kongo ikae meza moja na  M23 kwa ajili ya kutatua mgogoro wao, ulipokewa kwa mikono mwili na waasi hao, ingawa wametoa angalizo la kurudi tena kwenye uwanja wa mapambano iwapo watachokozwa.
Awali kiongozi wa kundi hilo la  M23, Betrand Bisiimwa, alipongeza uamuzi huo wa kuwataka wakutane na Serikali ya Kongo kwa ajili ya kutafuta suluhu ya mgogoro wao ambao umedumu kwa muda mrefu.
Bisiimwa akizungumzia uamuzi huo uliofikiwa hivi karibuni katika kikao kilichoketi Uganda, kilichowashirikisha Rais Jakaya Kikwete, Paul Kagame wa Rwanda, Joseph Kabila wa Kongo, Yoweri Museveni wa Kongo na wengine, alisema kikundi chake kilifanya juhudi kama hizo kwa zaidi ya miezi kumi iliyopita, lakini Serikali ya Kongo iliwapuuza, hivyo kusisitiza kwamba wapo tayari kwa mazungumzo au kuendelea na mapigano.
“Naupongeza wito wa viongozi wa Nchi za Maziwa Makuu kwa sababu wameona umuhimu wa kuyaokoa maisha ya Wakongomani wa hapa mjini Goma, siku zote amani inatafutwa kwa makubaliano ya kukaa meza moja, lakini ukiamua vita hauwezi kushinda,” alisema Bisiimwa.

Wednesday 11 September 2013




 Mkwanda amewahi kugombea ubingwa wa 
dunia wa IBF kwa vijana mara mbili.

 
 
Madawa ya Kulevya



Dar es Salaam: Bondia Rashid ‘Snake man’ Matumla amedai endapo itathibitika mdogo wake, Mkwanda anajihusisha kusafirisha dawa za kulevya atakuwa ameipa fedheha familia yao.
Matumla
Jicho la Habari
“Mkwanda ameipa fedhea familia yetu, hii ni aibu kubwa ukizingatia vitendo hivyo vinakatazwa si Tanzania tu bali na kwenye nchi nyingine,” alisema Matumla jana katika mahojiano na gazeti hili.
Mkwanda ambaye kwa mujibu wa Rashid alipumzika kucheza ngumi miaka kadhaa iliyopita kutokana na kusumbuliwa na  maradhi alikamatwa wiki iliyopita nchini Ethiopia akiwa na mchezaji wa zamani wa Simba, Joseph Kaniki na leo watapandishwa kizimbani nchini humo kwa tuhuma hiyo.
“Mimi mwenyewe nashangaa ni lini amejiingiza kwenye kazi hiyo, hata wakati anaondoka hakuniaga, mimi kaka yao na familia hatuelewi chochote,” alisema Matumla.
Alisema mdogo wake huyo alikuwa amebadilisha uraia na kuchukua uraia wa Sweden na kuoa hukohuko Sweden licha ya kwamba hapa Tanzania alikuwa amepanga Mbagala, Dar es Salaam na alikuwa anakuja na kukaa kwa muda na kisha kuondoka.
“Ni mwezi sasa umepita sina taarifa naye na hata wakati anaondoka hakuniaga, nimesikia kupitia vyombo vya habari kitendo cha mdogo wangu kukamatwa kimenisikitisha mno, siyo siri nimekwazika na ninarudia kusema hii ni fedheha kwenye familia yetu,” alisema bingwa huyo wa zamani wa dunia wa WBU. Rekodi zinaonyesha kabla ya kupumzika kwa muda kucheza ngumi, Mkwanda alishinda mapambano manane (sita kwa KO) alipigwa mara tatu zote kwa KO alitoka sare mara moja tangu 2004.

Wanasiasa kikwazo wahamiaji haramu






Dar es Salaam. Wanasiasa jijini wameshutumiwa kutokana na kuingilia mchakato wa kupambana na wahamiaji haramu unaondeshwa na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Dar es Salaam.
Kichefuchefu
chimbuko la wahamiaji haramu
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Said Meck Sadick alisema licha ya mchakato huo wa kupambana na wahamiaji haramu kuendelea vyema lakini wanasiasa hao wamekuwa wakiwakwamisha.
Alisema wanasiasa hao wamekuwa wakifanya mikutano usiku na wahamiaji hao kinyume cha sheria na taratibu na kuwapa moyo wahamiaji hao kuwa wasijali hakuna mtu atakayeweza kuwarudisha kwenye nchi zao.
“Operesheni hii tumeianza tarehe Mosi Septemba mwaka huu, lakini hawa wenzetu wanataka kutukwamisha kwa masilahi yao binafsi tunawaonya waache mtindo huu mara moja,”
 alisema
 Sadick.
 Nakuongeza kuwa;

“Baadhi yao tunawajua na tena wanadiriki kusema kuwa wahamiaji hao niwapiga kura wao ni raia halali wa Tanzania.

Tuesday 10 September 2013

Woman, be very afraid: Misogyny is reaching dangerous levels in Kenya





Ndege ya Tanzania



If Kethi Kilonzo and Gladys Shollei were men, would the Kenyan media and public have hung them out to
dry as they have been doing? Would the minutest details about their temperament and character have been the subject of discussion?
Would they have been tried, judged, and sentenced by the public before any evidence is presented? I seriously doubt it.
Similarly, if Nancy Baraza had been male and had pinched a female nose, would she have lost her job as Deputy Chief Justice? Maybe not. Because in Kenya powerful men can get away with murder, rape, sexual harassment, lying, and stealing, but if there is the faintest whiff of impropriety on the part of a woman, all hell breaks loose.
I am not saying that women are not capable of committing crimes or that they should not be reprimanded or punished for breaking the law; I am saying that the treatment meted out to women is very different from that meted out to men.
Kilonzo and Shollei are just two among many women who have learnt the hard way that there is nothing a Kenyan male fears more than a powerful woman. Last week, the social media was abuzz with news that Nairobi County Senator Mike Sonko had insulted radio presenter Caroline Mutoko on live radio.
This shocking news was followed by a video of Nairobi County Governor Evans Kidero slapping Nairobi Women’s Representative Rachel Shebesh outside his office.
Although Kidero quickly apologised for his actions, stating in his defence that the slap was a reaction to an assault on his lower abdomen, the fact remains that a man who represents four million Nairobians was seen hitting a woman.
Shortly after that episode, during an online discussion about the infamous slap and what it says to Kenyan women, a well-known hate-mongering individual, who ironically claims to have high regard for women, referred to me as “someone who thinks with her genitals”.
It seems misogyny in Kenya has reached unprecedented levels and cuts across all ethnic groups and classes.
Recently I wrote about a report that showed that levels of gang rape and murder of women and girls in Nairobi’s slums have reached epidemic proportions and virtually constitute a “femicide”. Misogyny, of course, is not a particularly Kenyan phenomenon; it exists in all societies where partriarchy prevails and where men fear the power of women.
The difference, I believe, is that in Kenya, misogyny has become normalised. The women’s movement (if we ever had one) is long dead. Women have been co-opted into the very male-centric patriarchal system that diminishes and destroys women.
Those women who still believe that if they work hard and prove their mettle, they will naturally rise to the top should just look at Kilonzo’s and Shollei’s cases and prepare for the day when they too will be judged and vilified by men who cannot bear the thought of women holding any kind of power or influence.
Dr Wambui Mwangi argues in a thought-provoking essay titled “Silence is a Woman”, published recently in The New Inquiry, that the domination of all Kenyan women by all Kenyan men is a post-colonial social contract that reinforces the patriarchal and ethnicist order.
This order states that if you are a woman, you are dispensable, that you do not really matter. Which is why there has been more outrage about the men who were killed or maimed in the 2007/8 post-election violence than about the women and girls who were brutally gang-raped.
Yet Kenyan women have in the past used the very bodies that Kenyan men despise to register political dissent. The Kenyan mothers of political prisoners who stripped in a section of Uhuru Park (now re-named Freedom Corner) used their bodies to make a political statement.
The late Wangari Maathai, who in my opinion was the only true feminist this country has known, suffered police beatings when she joined these mothers and when she tried to save Nairobi’s green spaces. She became a heroine abroad, but for all her efforts, was only appointed assistant minister by the Mwai Kibaki administration, an insult she bore with dignity.

TEMBO

Wanaswa na dawa za kulevya Ethiopia




Maporomoko ya Rusumo



Dar es Salaam. Mshambuliaji wa nyota wa zamani wa timu ya soka ya Simba na Taifa, Joseph Kaniki ‘Golota’ na bondia Mkwanda Matumla wanashikiliwa huku Addis Ababa, Ethiopia wakituhumiwa kusafirisha dawa za kulevya.
madawa ya kulevya
Bangi
Kukamatwa kwao kumezidi kuongeza idadi ya Watanzania maarufu waliotiwa mbaroni nje ya nchi katika siku za karibuni wakituhimiwa kwa makosa hayo.
Tukio hilo limetokea miezi miwili baada ya Watanzania wawili, wasanii Agnes Gerald Masogange na Melisa Edward kukamatwa kwenye Uwanja wa Oliver Tambo, Afrika Kusini wakituhumiwa kusafirisha dawa za kulevya zenye uzito wa kilo 150 na thamani ya Sh6bilioni.
Aidha, hilo limetokea baada ya meli ya mizigo ya Gold Star iliyosajiliwa nchini kukamatwa na maofisa Forodha na askari wa doria wa Italia katika Pwani ya Sicily, Bahari ya Mediterranean ikiwa na tani 30 ya dawa za kulevya aina ya bangi zenye thamani ya Pauni za Uingereza 50milioni (Sh125 bilioni).
Kaniki na Matumla walikamatwa Agosti 31, mwaka huu kwenye Uwanja wa Ndege wa Bole, Addis Ababa wakati wakijiandaa kupanda ndege ya Shirika la Ndege la Ethiopia tayari kwa safari ya kuelekea Paris, Ufaransa.
Kaimu Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia, Samuel Shelukindo alithibitisha jana kwamba wanamichezo hao wanashikiliwa nchini humo na Polisi wa Kitengo cha Uchunguzi wa Makosa ya Jinai.
Wanamichezo hao wamepandishwa kizimbani katika Mahakamu Kuu ya Ethiopia iliyoko kwenye eneo la Arada, Addis Ababa kujibu tuhuma za kubeba kilo saba za dawa hizo haramu. Mkwanda anadaiwa kubeba kilo nne wakati Kaniki akidaiwa kubeba kilo tatu. Kama watapatikana na hatia, wanaweza kufungwa kifungo cha miaka tisa hadi 15.
Alisema uwezekano wa kesi ya Kaniki na Matumla kurudishwa Tanzania haupo kwa kuwa nchi hizi mbili hazina utaratibu wa kubadilishana wafungwa.
“Wameshikiliwa hapa Ethiopia kwa zaidi ya siku 10 sasa, sisi tulipigiwa simu na polisi wa hapa Alhamisi iliyopita kujulishwa kwamba kuna Watanzania wawili wameshikiliwa kwa tuhuma za kukutwa na dawa za kulevya, tulipokwenda tukamkuta ni Kaniki na Matumla,” alisema Shelukindo.
“Wao wenyewe wanaeleza kwamba walipitia Mombasa na huo mzigo walipewa na mtu mmoja. Lakini Kaniki yeye anajitetea kwamba huyo aliyewapa huo mzigo pale Mombasa anajuana vizuri na Mkwanda. “Kwa hiyo alichofanya yeye ni kuubeba tu. Walikuwa wapitie hapa Addis wakashuke Paris, Ufaransa ndipo warudi Sweden kwa njia zao wanazojua wenyewe. Walipofika hapa Mkwanda alifanikiwa kupenya akapanda ndege lakini Kaniki akanaswa na mbwa ndipo akajitetea kwa polisi kwamba lile begi lilikuwa lake lakini mizigo mingine ilikuwa ya Mkwanda.
“Ndipo hapo sasa Mkwanda akashushwa kwenye ndege wakashikiliwa na Jumatatu ya wiki iliyopita wakapandishwa kwenye Mahakama ya hapa kutajiwa kesi yao lakini hawakupewa nafasi ya kujitetea. Kesi itatajwa tena Jumanne (leo) na Jumatano (kesho) na uchunguzi wa polisi bado unaendelea.”
Wanamichezo hao walidai kwamba walikabidhiwa mizigo hiyo kwenye Uwanja wa Ndege wa Mombasa walipokuwa wakikabidhiwa pasi za kupandia ndege baada ya kupita sehemu zote za ukaguzi.


“Kilichotokea ni jambo la aibu kwa nchi na hata wachezaji wenyewe wanajuta. Kwa mfano, Kaniki anasema alikuwa aende England kucheza mpira Desemba lakini sisi tukamwambia hatuwezi kumsaidia inabidi akabiliane na kesi iliyoko mbele yake. Mkwanda yeye ametuambia kwamba anaishi Sweden hatuna maelezo yake zaidi,” alisema Shelukindo na kuongeza kuwa wamewapelekea wanamichezo hao msaada wa mablanketi kwa vile bado wako mahabusu na Ethiopia kwa sasa kuna baridi kali.
Shelukindo alisema wachezaji hao wapo mahabusu kwenye Kituo cha Polisi cha Uchunguzi wa Makosa ya Jinai (Federal Police Crime Investigation) na hawana chochote zaidi ya nguo walizokuwa wamevaa.
Watanzania wengine kuachiwa leo
Shelukindo alisema kuna Watanzania wanne wanaotazamiwa kuachia leo baada ya kumaliza vifungo vyao baada ya kupatikana na hatia ya kusafirisha dawa za kulevya.
“Kuna Watanzania wengine walinaswa hapa miaka ya nyuma wao walikuwa wamemeza wakapasuliwa dawa zikatolewa na baadhi yao walifariki. Hata hivyo, wanne ambao wamemaliza vifungo vyao vya miaka minne wanaweza kurudishwa Tanzania,” alisema Shelukindo.

Twiga mdogo

Monday 9 September 2013

‘Wahamiaji walioolewa ruksa kuishi na wenza’



 
Kilimanjaro   



 OPARESHEN KIMBUNGA

Bukoba. Serikali imesema wahamiaji haramu walioolewa na Watanzania wanaruhusiwa kubaki nchini, hawalazimiki kuvunja ndoa zao ingawa wanatakiwa kupata kibali maalumu kutoka Idara ya Uhamiaji.
Akizungumza mjini hapa jana, Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Kanali Mstaafu Fabian Massawe, alisema wahamiaji haramu walioolewa wanatakiwa kwenda Idara ya Uhamiaji kupata hati hizo.
Rusumo
Kikosi kazi
“Hatupendi kuachanisha familia zilizoishi kwa zaidi ya miaka miwili mfululizo, wanatakiwa kwenda uhamiaji kuhalalishwa na baadaye ikigundulika hana tatizo anaweza kupewa uraia,” alisema Kanali Massawe.
Pia, alisema kwa mujibu wa sheria, mhusika atapewa kibali alichokiita ‘Independence Pass’
kitakachomwezesha kuendelea kuishi  nchini na kwamba, kinyume chake itakuwa ni kuvunja haki za binadamu.
Hata hivyo, Massawe alibainisha kuwa lazima zoezi la kuondoa wahamiaji haramu lifanyike, kwani walioondoka kwa hiari ni 11,601 na waliokadiriwa kuondoka ni kati ya 52,000 na 53,000, hivyo idadi kubwa bado wanaishi nchini.
Maafisa Uhamiaji
Akizungumzia zoezi la kurudisha wahamiaji haramu lililoanza rasmi Septemba 6, mikoa ya Kagera, Geita na Kigoma, Mkuu Msaidizi wa Operesheni hiyo, Simon Sirro, alisema tayari wamewakamata  1,851.
Pia, Sirro alisema ng’ombe 1,765, sare za Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) na bunduki saba vimekamatwa  na kwamba, wahamiaji  wanaokamatwa wanarudishwa kwa mujibu wa sheria kwa kuzingatia haki za binadamu.