Sunday, 21 April 2013

Viongozi walioongoza idara ya Uhamiaji -1961 ...2013

 Hama tunavyo jionea ramani yetu ta Tanzania na viongozi wake walio hudimia idara ya Uhamiaji Tanzania ni kama wafuatao:-kuanzia mwaka 1969 hadi 1993

(1)....Mh.Raphael Kubaga... mwaka 1969 hadi 1983
Afisa Uhamiaji Mkuu,

(2)....Mh.Mbwana Mohamedi Bakari ...mwaka 1983 hadi 1989
Mkurugenzi wa Uhamiaji

(3)....Mh.Ali A Mnyika.... mwaka 1989 hadi 1993
                                                   Mkurugenzi wa Uhamiaji
hawa ni viongozi wa kwanza katika idara ya Uhamiaji na ndiyo walio ichukua idara na kuwa kabidhi viongozi wenzao waliotuleta hadi hivileo....


(1)....Mh:Judith Mtawali Kuanzia ..mwaka 1993 hadi 1997
Mkurugenzi wa Uhamiaji,

(2)...Mh:Kinemo D. Kihomano...Mwaka 1997 hadi 2010
Mkurugenzi wa Uhamiaji,

(3)...Mh.Magnus P. Ulungi...Mwaka 2010.............

nivyema tuwajue na kuwakumbuka kwa kazi yao nzuri walio ifanya mara tu baada ya Uhuru hadi hivileo....Tuna wapongeza sana....................................................................

SENENE...wa mkoani Kagera

MWAE ziwani victoria
  Napenda kukitambulisha kivutio hiki cha ajabu katika ziwa letu hili la la Victotia haya ni mawe makubwa yaliyo jipandikiza juu ya mawe haya makubwa yenye uvutio mkubwa katika ziwa hili la victoria tukiweza kusema yakuwa Tanzania tumepata upendeleo mkubwa kutoka kwa Mungu mawe haya ni sehemu ndogo tuu ya kivutio hiki katika ziwa hili lililo sheheni samaki wakubwa, aina ya Sangara, Terapia, na wengine wengi waliomo ndani ya ziwa hili lakini kwaleo ningependa kukutambulisha kisiwa kilicho pombezoni mwa mwalo wa Bukoba kijulikanacho kwa jina la Kisiwa cha  KEREBE, kisiwa hiki kipo usoni mwa mji wa Bukoba na ukisimama katika kiwanja cha ndege cha Bukoba utakiona kikijitokeza kwa upanda wa kushoto mwa uwanja huu

KEREBE: na mialo ya mji huu wa Bukoba ni mazalio makubwa wa panzi hawa maarufu wajulikanao kwa jina la SENENE senene ni aina ya panzi wanao kuja kwa msimu wa majira ya mvua zinazo nyesha humu mkoani kwaetu Bukoba na kagera kiujumla panzi hawa wamekuwa wakipewa hesima kubwa kwa wenyeji hawa wa mkoa huu wa kagera wameweza kutumika kama zawadi kutoka kwa Mungu na wamekuwa wakitumika kwa kutumiana aidha kwa watu wapenda nao kuonyesha hali ya kukuthamini wewe utumiwao...zawadi hii hufungwa katika majani ya migomba ilio andaliwa vizuri na yenye kutoa mvito kwa utumuwae.

SENENE: mara watakapo pokelewa kwa mtumiwae na yeye alie kabidhiwa atapaswa kurudisha shukurani kama vile kanga, kitenge na kadharika

BUKOBA: mara senene hao wakamatwapo hutayarishwa kwa kuchemshwa na kuanikwa kwa muda mpaka watakapo kauka na kuhufadhiwa ....lakini kunawengine hutolewa mabawa na kuwekewa viungo mbalimbali ili kuongeza radha kwamfano pilipili, kitunguu/ kitunguu saumu binzari nk. hii ni katika kuongeza radha tuu kiujumla ni burudani tipu huko mkoani kwetu KAGERA njoo ujionee vijimambo vya mkoa huu wa Kagera.

Saturday, 20 April 2013

MNYONGE MNYONGENI LAKINI HAKI YAKE MPENI...

SIMBA
 Hivi kwenye ukweli kwanini uongo usijitenge huyu bwana ni mfalme wa poli na alipokea sifanyingi sana za kolini na binadamu yakuwa yeye ndiye mfalme wa poli wengine walimwita nikiboko wa njia akivimba hapapitiki au wengine walidai yakuwa hawezi kuzoeleka na kutu chochote na hawezi kuchekewe na kiti chochote.....aaaaaaa! huo ni uongo msemakweli ni mpenzi wa mungu hebu tazama sasa mfalme wa poli akichezewa sharubu na huyu simba jike kwahiyo ile dhana yakuwa huyu bwana ni kuboko ya wote ni uongao nayeye ana kiboko yake .....na hawezi kufurukuta katika mahusiano haya yaliyo pangwa na mungu ....hatamimi na wewe hakuna awezae kujua dhana hii imepeperushiwa wapi kati wa hahasimu hawa wawili kwakweli ajuaye ni mola tuu kwa kweli fumbo hili ni lazima tumuachie mungu hivyo nivyema tumjiue mungu kwania yeye ndiye mfumbuzi wa yote
KIBOKO

Sasa ona mwanadamu alivyo kuwa mnafiki ni muda mchache alikiri yakuwa simba ni kiboka wa yote hivi kwa hili ni nani wa kupongezwa yakuwa ni msema ukweli sasa kiboko ni mnyama mpole sana na ameamua kumfungia kazi mwanadami na kumwonyesha nayeye anayawezi...".KWAKWELI YOTE YANAWEZEKANA MBELE YA MUNGU"

KIJIJINI KWETU....Mandera , Kwamagome....ya Tanga

ndugu na jamaa -kijijini Mandera
 Matembezi yangu mkoani Tanga nilitembelea kijijini kwangu Mandela na Kwanmagome Handeni Tanga nilikaruibishwa na nduguzangu , jamaa marafiki wote walifurahia ujiu wangu na kukumbushana mengi ya miaka ya nyuma iliyo pita tulitembelea maeneo ya kijijini kwetu , tulisalimiana na ndugu tulikunywa na kula kwa pamoja.....





KIJIJI CHA MANDELA  KIPO WAPI? HUKO MKOANI  TANGA?
Kakweli kijiji cha Mandera kipo Mkoani Tanga Wilaya ya Handeni kijiji cha Mandera na ukitaka kukikifikia itakibidi utoke mjini Handeni na uwe ukielekea njia ya kwenda Korogwe itakuchukia kati ya dakika 30 au 4
kijiji cha mandera
 45 kukifikia kijiji hicho unapotoka Handeni utaelekea stendi ya Chogo ambayo ni stendi ya mabasi ya Handeni utakwenda moja kwa moja hadi ukitane na njia panda mpya ya kutokea Chanika ya Handeni ineyo unganika na ya kwenda Korogwe utakwenda kwa muda wa dakika kadhaa ndipo utakapo iona barabara wa vumbi upande wa kushoto ukiwa ukielekea Korogwe utapinda na kuendelea na njia hiyo ya vumbi kwa muda wa takribani wa dakika 15 niyo ukutane na kijiji hicho cha MANDERA sasa ukienda mbele zaidi utajikuta ukielekea kijiji kingine cha KWAMADULE huko ndiko wazaza wangu waliko tokea.....kijiji hiki kilisifika sana kwa kuwatoa wazee walio tumikia selikari ya awamu ya kwanza wakiwemo walimu askari na wakuu wa idara nyingine nyeti katika nchi hii .....huo mti unao uona ndipo palipokuwa mji wetu wa zamani
kijiji cha kwamagome

...Kijiji cha kwamagome tilipata bahati ya kuku tembelea nako tulipata mapokezi ya kufa mtu tulikula na kunya kwa pamoja na kufurahia ndhari nzuri ya kijijini kwetu kwamagome nikweli " MKUMBUKA KWAO SI MTUMWA"...Nawakaribuisheni kijijini kweti HANDENI......Mjioneee.

NENO NGARA MAANAYAKE...

Mingara
Poli la kimisi lipo mpakani mwa wilaya ya karagwe ukielekea wilaya ya Ngara kabla ya kufika njia panda ielekeayo Ngara, na mpakani mwa Tanzania na Rwanda-Rusumo, utakutana na njia panda ya Benako hapo utakuwa umeingia walaya ya Ngara njia huu ya benako kuelekea Rwanda inapirika pirika nyingi za ujenzi wa taifa utakutana na magari mengi ya mizigo abiria, na hata ya binafsi yanayo ingia na kutoka Ngara kuelekea Rusumo au yanayotokea Rusumo kwenda Ngara.......lakini kwanini nimependa kisemea hili? mimi binafsi nimevutiwa sana na Hadithi hii ya wenyeji wa Wilaya hii ya Ngara ambao walinihabarisha kuhisiana na Neno hili la mji huu wa Ngara kumbe lina maana ya mti mmoja unao onekana katika Wilaya hii ya Ngara mti huu unahesimiwa sana wenyeji wa wilaya hii wajulikanao kwa kabila la, wahangaza na si mwingine bari ni Mngara huu mti una matawi yaliyo jiachia kama mwamviri na yenye majani madogo madogo yanayo onyesa sura nzuri ya mti huu uliotoa jina la wilaya hii ya Ngara.....ukitaka kujua mengi Tembelea Ngara ujionee....


Barabara inayokatisha pori la kimisi mbele kidogo upande wa kilia kama unaelekea Ngara utaliona ziwa chamchuzi ziwahili linapakana na nchi ya Rwanda,
Pori la kimisi
hapo ukiambaa na mpaka wetu huu utakutana
na maporomoko ya maji eneo la RUSUMO.
au Rusumo foll's.....hapa najaribu kukupa picha na kutaka kuku habarisha chanzo cha Mto Kagera
ulipo patia jina hili ni mkoana Kagera..makutano haya utayapatia Katika daraja linalo unganisha,
nchi ya Rwanda na Tanzania pale pana maporomoko sasa muungano wa Mto Ruvuvu, Na Akanyaru....Mto Ruzvuvu mto huu unatokea Nchini Burundi Kupitia pembeni kidogo na Kabanga na Rulenge....Mto Akanyaru hutukea ndani ya Rwanda na yete miwali inakuja kukutana maeneo ya Rusumo ....na kuangukia darajani Rusumo mbelekidogo tuu mto huu hubadilika jina na kuitwa Mto kagera .....mto huu maji yake hubadirika rangi na nikutokana na yanaku tokea mvua zikunyesha Rwanda Akanyaru unaleta maji mekundu......Mvua zikinyesha Burundi Ruvuvu utaleta maji meusi haya ndiyo maajabu ya mto kagera yanapo tokea....njooo ijioneee.

Friday, 19 April 2013

kagera sugar...kagera sukari


KAGERA SUGAR-(KAGERA SUKARI)

TUNAPO SEMA:- Kagera Sikari au Kagera sugar ni kampuni ya utengenezaji sukari mkoani kwatu KAGERA…. kwakweli nimepaswa kulisema hili kwakuwa kumekuwepo na dhana ya kuwa mambo mzuri yote yapo mijini… kwakweli usemi huu ulifutwa na marafiki zetu kutoka Australia na mwingine kutoka marekeni ambao walidiriki kusema yakuwa.
 kuwanda hiki cha sikari Tanzania ni hazina ya utajiri iliya jificha katika kiza kinene”  mimi nilifanikiwa kumuuliza kwanini unasema hivi?
   wao wakanijibu “unasikia rafiki ….wewe hujui” kwani nitakueleza na wewe utaamini ….unajua kiwanda hiki kinatumia fedha nyingi katika kuanda sukari tu…  wakacheka na kusema “sukari tuuu” wakaendekea kusema huku wakiwa makini zaidi hiki kiwanda mimi nakuapia ni pesa tupu pesa peesa pesa tupu, alisistiza huku akiashiria kuomba apatiwe kiberiti cha kuwashia sigareti yake….akaanza kutujuza huku… akiiwasha sigareti yake….ona

Unafahami katika mua kunautajiri mwingi sana kwa mfano:-
ü  Muwa:- tuu yale majani yake…..utapata chakula cha wanyama kama vile Ng’ombe, Sungura, farasi, mbuzi, nk. Alisema mmoja wa marafiki hawa alisema,
ü  Molases:-aliemdelea  kusema hii ipo katika aina ya tope zita lenye rangi nyeusi likiandaliwa vizuri lingeweza kutoa spiriti nyingi sana ambayo mngeweza kutengenezea vinywaji vikali ambavyo vinge tengenezwa kitaalamu na vitawaburudisha wananchi, isitoshe pia mahospitarini spiriti hii ingefaa, sasa ona wangepata pesa ningi watakapouza nje ya nchi hivi mnaonaje marafiki sisi tulikaa kimya tukimkodokea macho akaemdelea kusema.
ü  Mbolea:-aliendelea kusema unajua matakataka waliozalishwa na utengenezwaji wa sukari au ya miwa hii ingeweza kusindikwa kwa muda furani hadi yakawa mbolea ambayo yangetumika katika kukuzia mazao ya mashambani na katika bustani zetu za mboga au maua kitu ambachu watu wangegombania na kuwaingizieni fedha nyingi mifukoni mwenu rafiki aliendelea kuelezea.
ü  Gasi:-aliendelea kusema yakuwa hii miwa na uchafu wake ukiuhifadhi kitaaram unaweza kupata gesi nyingi ambayo mngeweza kuitumia katika matinizi yenu kama ya kupikia na hata kuwashia taa katika vijiji vyenu,
ü  Vinywaji:-alisisitiza kwa kusema yakuwa mimi napenda sana kunywa juisi hapa kunaaina nyingi za vinywaji, tangu vya baridi hadi vya moto! Alicheka na kutuomba tumruhusu aendelee na safari yake.

Tulishikwa na butwa tusielewe la kulichangia katika mazungumzo hayo tuliwaaga marfiki zetu hawa na kuendelea na safari yau kurudi kwao….kwakweli mashamba ya Kagera sugar, kimwonekano ni hazina kubwa mkoani kwetu kagera na nikivutio kikubwa sana sana kama hauamini ngojea nikitumie japo picha hizi nawewe uweze kuburudika kama sisi wenzio tunavyo farijika na hazina hii tuliyo nayo huku kwetu Kagea……leo nakuonyesha kwa kiasi tuu sikunyingine nitakuonjesha hata sukari yetu ya Kagera sugar….

Wednesday, 17 April 2013

CHAKULA CHA KITANZANIA...UGALI KWA MCHICHA



CHAKULA CHA KITAMZANIA

Napenda kukitambulisha chakula hiki kitamu cha Kitanzania hapa pana ugali, listi nyama, Dagaa wa kupwaza ….. mchicha ugali mweupe uliopikwa kwa kiasili wa Kitanzania maandalizi yake ni vyepesi tuu tukianzia kwa uandaaji wa ugali:

UGALI:  Andaa unga mweupe wa kutosha andaa maji ya moto mekoni (jikoni) baada ya maji kuchemka weka unga kwenye maji yanayo chemka anza kusonga hadi unga na maji yachanganyike na unga ule ulio uweka katika maji yale yalio chemka na kukuonyesha mchanganyiko ule umekamilika na kukuonyesha yakuwa mchanganyiko ule umeiva kwahiyo huo utakuwa ugali umeiva.


MCHICHA: Andaa mchicha vitunguu, nyanya, Mafuta au karanga tui la nazi tenga mchicha huo jikoni kwa muda utaona maji yakitoka kwenye mchicha ule na mchicha ule kuanza kubadilika na kuwa rangi ya kijani na kujitokeza maji chemsha kwa muda mfupi…..toa mchicha wako jikoni weka sufuria nyingine jikoni weka mafuta, karanga au tui la nazi. Kama ni kwa mafuta kaanga vitunguu weka chumvi kwa muda mfupi weka mchicha changanya hadi urudhike mchanganyiko huu upo sawa hapo itakuwa imeiva…….

DAGAA WA MCHUZI: Tayarisha dagaa wako wakavu kwa kuwakosha na kuwaondoa uchafu wakaange kwa muda mfupi na zisikauke sana weka nyanya vitunguu hakikisha mchanganyiko huo unaiva vizuri hadi kuonyesha mchanganyiko huo umeiva hapo ndipo utakapokuwa mwisho na mwanzo wa kuliwa….tenga vuzuri chakulahicho cha kitanzania na anzakula ni chakula kitamu sana hasahasa ukishushia kwa maji  ya baridi.